MST-Department of Kiswahili and African Languages

Permanent URI for this collection

Browse

Recent Submissions

Now showing 1 - 20 of 258
  • Item
    Ubora wa tafsiri katika kamusi tafsiri za mtandaoni
    (Kenyatta University, 2024-06) Lukungu , Winnie O.; King'ei, Kitula Osore, Miriam
    Kiswahili ni lugha inayozidi kukita mizizi kidijitali kupitia mbinu anuai ikiwemo programu za kamusi na vitabu vingine kama Bibilia vilivyoswahilishwa na kuhifadhiwa mtandaoni. Utafiti huu ulinuia kudihirisha ubora wa tafsiri ya maneno yaliyotolewa katika kamusi-tafsiri za mtandaoni. Kwa kuwa enzi hii kuna watumizi wengi wa mtandao kwa malengo anuai, kamusi za mtandaoni zina dhima kuu na hivyo kuwepo na tafsiri potovu kunaweza kuwaathiri watumiaji wengi. Utafiti ulichukua muundo wa kutathmini tafsiri ya maneno kwenye kamusi zilizoteuliwa za mtandaoni kuanzia alfabeti A – M na kutoa mapendekezo ya tafsiri bora zaidi, kwa msaada wa wataalamu wa lugha kama vile waandishi wa kamusi kama walivyolengwa na mtafiti. Mtafiti alishirikiana moja kwa moja na wataalamu hawa kama vile waandishi wa vitabu mbalimbali na wanaotumia kamusi hizi katika kuandaa tasnifu yake kupitia kwa mahojiano, hojaji pamoja na mawasiliano ya kila mara kupitia simuni ili kuhakikisha kuwa malengo yake yametimia. Utafiti huu ulilenga tafsiri ya Kiingereza-Kiswahili na wala sio lugha zingine. Mihimili ya Nadharia ya Isimu Kongoo ilitumika katika kupendekeza kongoo matini bora inayotumika kama tafsiri kwa kamusi za mtandao. Mbali na nadharia hii, nadharia ya Ulinganifu wa Kimuundo ambayo ni mojawapo ya miavuli ya nadharia ya Tafsiri ilitumika katika kuasisi tafsiri bora kwa maneno. Utafiti ulikuwa wa kimaelezo, na usampulishaji wa kimakusudi ulitumika katika kuwateua wahojiwa pamoja na kuteua data kutoka kwenye kamusi za mtandao. Data ilichanganuliwa kwa mwongozo wa mihimili ya nadharia pamoja na malengo ya utafiti. Baada ya kuchanganua data, matokeo yaliwasilishwa kwa kutumia maelezo na michoro ya jadwali kisha kutolewa maelezo yake. Matokeo ya utafiti yananuia kuboresha tafsiri ya kamusi kwenye mtandao ili kuwafaidi wategemezi, waunfaji na watumiaji wa kamusi hizi katika shughuli zao anuai. Baadhi ya watakaoweza kufaidi kwa kamusi yenye tafsiri bora ni pamoja na wasomi, watafsiri, walimu, pamoja na wageni wanaotumia kamusi hizi ili kujifundishia lugha ya Kiswahili.
  • Item
    Maana Kimatilaba katika Matangazo ya Kibiashara ya Kiswahili kwenye Televisheni
    (Kenyatta University, 2024-06) Mucee, Geoffrey Mutinda; King'ei, Kitula Osore, Miriam
    This research evaluated the connotative meaning of the Kiswahili television advertisements in Kenya. The research identified various televised Kiswahili advertisements with negative connotative meaning, analysed the televised Kiswahili advertisement texts with negative connotative meaning and discussed how the viewers of the televised Kiswahili advertisements interpet these advertisements. The study was guided by the tenets of Semiotic theory. The theory advances the relationship between a sign, an object and a meaning. The data for the research was generated from the Kiswahili advertisements with connotative meaning. Aspects of connotative meaning from the televised advertisements has been identified and sampled purposively. The research has been conducted from both the library and the field. The researcher has interviewed various advertisement viewers in order to identify how they perceive the the televised Kiswahili advertisements that have connotative meaning. The research was also carried out in the library where literatute review of books, journals and a variety of theses related to the topic of research to give this research a basis was done. Data was collected based on the research objectives and analysis of the data was guided the Semiotic theory. The presentation of the study findings was through narration where relevant examples were used and a summary given thereafter. The study established that the Kiswahili television advertisements in the study had negative connotative meanings that resulted in negative reactions. The study also found that the use of language, picture, and video signs in the Kiswahili television advertisemnets had negative connotations that elicited negative feelings. Also, the study established that majority of viewers of Kiswahili television advertisements view them as having the potential to elicit negative and positive feelings which can affect their perspectives of certain products, servives and or the behaviours of people in society. This study hopes to benefit researchers and scholars of Swahili semantics. This is because it will shed light as far as negative connotative meaning from televised Swahili advertisement is concerned.
  • Item
    Utatuzi wa Makosa ya Kimofosintaksia Miongoni mwa Wanafunzi Wazawa Wa Lubukusu Wanaojifunza Kiswahili Sanifu, Kaunti Ya Bungoma, Kenya
    (Kenyatta University, 2024) Namunyu, Emmanuel Wafula; King'ei, Kitula Osore, Miriam
    This research explored intervention measures to Morphosyntactic errors among the native Bukusu learners of Kiswahili. It purposed to confirm the existence of these errors among the learners as claimed by the preceding researches, evaluate the teachers’ intervention measures, and finally suggest the appropriate intervention measures to correct them. It was guided by the Theory of Interlanguage (TIL) and the Theory of L2 learning by Krashen. The IL refers to the type of language produced by learners of L2 which is neither TL nor NL. It asserts that the language of learners goes through various stages before reaching perfection in their L2 production skills. This research is qualitative. The researcher adhered to the field procedure in collecting data. Learners were given an exercise to write a composition on the same topic and fill in the blank spaces. The researcher also listened to their oral narratives to have a glimpse of their spoken language to make a worthwhile conclusion. The research involved forty students from four day secondary schools in Bungoma Central Sub-County which included Musokho Friends, Sichei Friends, Chebunyinyi A.C.K and S.A Wabukhonyi. Four teachers of Kiswahili: one from each of the four schools were also involved to evaluate their intervention strategies. Data collected was analysed by exposing the errors, categorizing them, exposing their sources, evaluating teachers’ intervention measures and recommending appropriate intervention measures. Data collected was systematically presented through explanations and tabulations in various chapters of the entire work. Not only will this research benefit teachers and learners, but also the authors of grammar course books by ensuring their books meet the learners’ needs. We hope that curriculum developers could also benefit from it as they would arrange the grammar concepts in a way that makes it easy for the learners to comprehend having realized the learners’ problems.
  • Item
    Ukiukaji wa Kanuni Bia za Greenberg Katika Miundo ya Tungo zenye Vihusishi Katika Lugha ya Kiswahili
    (Kenyatta University, 2024) Ongwae, Jemimah Kwamboka; King'ei, Kitula Osore, Miriam
    This research investigated the violation of some of Greenberg’s linguistic universals in structures with Kiswahili adpositions. The research is derived from the field of linguistic typology. This field aimed at researching and analyzing the common properties and structural diversity for grammatical phenomena across the world`s languages. We followed Greenberg’s (1963) proposed set of 45 linguistic universals based primarily on a set of 30 languages considering the measure of orderliness of grammatical constituents in different language families. Kiswahili language was among the languages considered in his sample. Even so, it seems that some non-implicational universals proposed by Greenberg do not exist in the definitional characteristics of this language because Kiswahili got both prepositions and postpositions. This study focused on achieving the following objectives: It described the specific positions in which adpositions appear in sentences, to scrutinize different prepositional and postpositional structures and how they affected the structure of sentences and analysed the linguistics environments that trigger the violation of some of Greenberg’s universals in structures with Kiswahili adpositions. This research was guided by X-bar theory of Chomsky (1970). This is a substantive theory that analyses phrase structure properties of natural languages. Greenberg`s universals of language were also used too. Research data was Kiswahili prepositions which were collected by purposeful sampling method by reviewing literature from grammar books, journal articles and the other internet materials. Data analysis and presentation was based on the objectives through descriptive content analysis. This research revealed that when prepositional incorporation occurs to governing verbs, it affects the structure of the sentence by removing the preposition and causing displacement of the direct object. We were also able to determine that Kiswahili is a language of adpositions. However, when prepositions are placed between two nouns, especially when a-conjuctions are analyzed in X-bar theory, Kiswahili seems to be a prepositional language. Some of Greenberg’s universals were violated in Kiswahili structural sentences due to to Kiswahili language having both prepositions and postpositions. Although it was also revealed that some of Greenberg’s universals bring some validity and compliance in the Kiswahili language. The study has contributed to the copus on word order, typology of languages and Kiswahili syntax. It has benefited grammarians and linguistics researchers interested in structural analysis, especially Bantu linguistics.
  • Item
    Mchango wa Sitiari na Metonimu Katika Uzuaji wa Polisemia Katika Kiswahili
    (Kenyatta University, 2024-04) Masika, Mark Elphas; King'ei, Kitula Osore, Miriam
    Utafiti huu ulilenga kuangazia mchango wa sitiari na metonimu katika uzuaji wa polisemia katika Kiswahili ambapo uliweza kupambanua namna metonimu na sitiari zinavyoweza kuzua maana mpya ya maneno ya Kiswahili. Pia ulitusaidia kufahamu athari ya metonimu na sitiari katika uzuaji wa polisemia katika Kiswahili. Kimsingi polisemi ni leksimu moja yenye maana nyingi ambazo zinahusiana kwa njia moja au nyingine (Chacha na Pendo, 2019). Pia kuna njia zingine za uzuaji wa polisemi kwa mfano ukopaji, mabadiliko katika matumizi ya neno, na ufasiri mpya wa homonimu. Kuna baadhi ya wataalamu ambao wamezungumzia polisemia kama vile Mwendamseke (2016) aliyeandika makala kuhusu uelekeo wa maana za kipolisemia katika msamiati wa Kiswahili. Naye Gaichu (2013) alishughulikia uchunguzi wa sitiari dhanifu katika methali za Kiswahili. Utafiti huu wa sitiari na metonimu ndio usiodhihirika moja kwa moja. Utafiti huu uliongozwa na malengo yafuatayo: Kubainisha polisemi ambazo zimeundwa kutokana na sitiari na metonimu katika Kiswahili, kuainisha polisemi katika lugha ya Kiswahili, kudhihirisha mchakato ambao sitiari na metonimu hupitia kuunda polisemi katika Kiswahili. Nadharia ya semantiki tambuzi iliongoza utafiti huu. Nadharia hii ni sehemu ya nadharia ya Isimu Tambuzi ambayo ina misingi katika saikolojia tambuzi (Vyvyan & Greens, 2006). Data husika ilikusanywa maktabani. Maktabani, maneno ambayo ni polisemi na yameundwa kwa sitiari na metonimu kwenye Kamusi ya Kiswahili Sanifu (2018) yalikusanywa. Mbinu ya usampulishaji wa kimaksudi ilitumika katika uteuzi wa sampuli. Data ilichanganuliwa na kuwasilishwa kwa njia ya kimaelezo na majedwali ili iweze kueleweka. Kutokana na data ya utafiti huu, imebainika kuwa kuna baadhi ya polisemi zilizojitokeza ndani ya homonimu. Kwa mfano, tata2 na chuo1. Pia, imebainika kuwa data hiyo ilikuwa na polisemi za majina ya wanyama, wadudu na ndege. Hata hivyo, imebainika kuwa sitiari huwa na maeneo mawili ya ufahamu: moja ni ile inayotokana na maumbo tunayoyaona na nyingine ni ile ya kidhahania. Hiyo ya kwanza inaitwa eneo chasili na ya pili eneo lengwa. Kwa mfano, sitiari “Maria ni chui” maumbo tunayoyaona (eneo chasili) ni Maria na chui na maumbo ya kidhahania (eneo lengwa) ni ukali. Kwa upande mwingine, imebainika kuwa metonimu huwa na eneo moja. Kwa mfano, leksimu kiti eneo lake ni uongozi. Tafiti zingine zinaweza kufanywa kuhusu mchango wa mbinu zingine za lugha kama vile tashibihi, lakabu na jazanda yaani; namna ambavyo mbinu hizo zinaweza kuchangia pia katika kuunda polisemia katika Kiswahili.
  • Item
    Uanuwai wa Kimofolojia Katika Tafsiri za Nomino za Pekee Katika Biblia
    (Kenyatta University, 2023-06) Mwangi, Simon Kiarie; Leonard Chacha; Miriam Osore
    Abstract
  • Item
    Mchango Wa Kiswahili Katika Mofofonolojia Ya Nominomkopo Za Kibukusu
    (Kenyatta University, 2023-06) Juma, James Tom; Jacktone Okello Onyango
    Abstract
  • Item
    Changamoto Katika Ujifunzaji Fonolojia Arudhi ya Kiswahili Katika Shule za Upili, Gatuzi la Homabay, Kenya
    (Kenyatta University, 2023-05) ‘Wagabi, Wanga James; Jacktone O. Onyango
    Abstract
  • Item
    Usawiri wa Waathiriwa wa Ghasia za Kisiasa na Kijamii katika Riwaya Teule za Kiswahili
    (Kenyatta University, 2023-11) Mogondo, Erickson Okora; Beth N. Mutugu.
    Abstract
  • Item
    Uchanganuzi wa Makosa ya Kisarufi Katika Insha za Kiswaiiele Miongoni Mwa Wanafunzi wa Shule za Upili Katika Kaunti ya Nakuru Kenya
    (Kenyatta University, 2023-11) KIGIA, JOHN MWAURA; Babusa Hamisi; Miima Florence
    Abstract
  • Item
    Uchanganuzi wa Nyimbo za Jaguar (Charles Njagua Kanyi) na Willy Paul (Wilson Abubakar Radido)
    (Kenyatta University, 2023-06) Ng'ata, John Gituhu; King'ei, Kitula Osore, Miriam; Richard. M. Wafula
  • Item
    Uchanganuzi wa Nyimbo za Jaguar (Charles Njagua Kanyi) na Willy Paul (Wilson Abubakar Radido)
    (Kenyatta University, 2023-06) Ng'ata, John Gituhu; King'ei, Kitula Osore, Miriam; Richard. M. Wafula
  • Item
    Mbinu za Kujllmarisha na Kujidumisha Kilugha kwa Wambeere
    (CHAKAMA, 2015) Kaviti, Fridah M; Ngugi, Pamela
  • Item
    Isimu Ikolojia ya Leksimu za Miti Shamba Katika Lugha ya Kiswahili
    (Kenyatta University, 2023-11) Karoli, Bonareri Nelly; Leonard Mwita Chacha
    This study examined the ecology of herbal lexicon in Swahili language. Ecology is a branch that explores debates that are relevant or inappropriate for the environment. Language and culture are inseparable. Language patterns influence the way humans think about their environment and that leads to actions that are the heart of the ecological challenges they face. In this project, we analysed how herbal lexicons are considered as signs of environmental conservation techniques in the ecosystem. The project aimed to achieve these goals: to identify how the herbal lexicons could be classified in the Swahili language, to examine how the herbal lexicons reflected environmental conservation and to demonstrate the relationship between the herbal lexicons and the Swahili culture. This study was guided by the ecosemiotic theory that helped us understand that what is identified as an impact on ecology often has semiotic factors and differences in interpreting signs or vocabulary. Data was collected by the interview technique from the Swahili speakers found in Mvita. We noted that there are herbal lexicons like mpambamwitu that the Swahili used to show the beauty of their forests by bringing a natural image and a unique look. In addition, we found that the Swahili people interacted with the herbal trees in their day-to-day life such as mwarubaini. This culture was seen as a system of symbols that the Swahili used to communicate and bring meaning to their environment. How we choose our vocabulary while communicating about the environment can change the way the community views their environment. This study suggests that we should recognize the value of the natural environment and incorporate it into our policies and systems. By recognizing that our environment is our biggest ally then we will use it in a sustainable way for future generations. 1
  • Item
    Athari za Ekegusii Katika Matumizi ya Kiimbo cha Kiswahili Miongoni mwa Wanafunzi wa Shule za Upili Kaunti ya Kisii, Kenya
    (Kenyatta University, 2023-11) Nyougo, Christine; Peter Githinji
    Utafiti huu ulichunguza matumizi ya kiimbo cha Kiswahili miongoni mwa wanafunzi wanaozungumza Ekegusii kama lugha ya kwanza. Shule tatu zilihusishwa katika utafiti huu: Shule ya upili ya Senior Chief Musa Nyandusi, Nyamondo na Nyabisia. Malengo ya utafiti huu yalikuwa: Kutathmini utamkaji na ufasili wa kiimbo cha Kiswahili miongoni mwa wanafunzi wanaozungumza Ekegusii kama lugha ya kwanza, kuchunguza jinsi viarudhi vya lugha ya Ekegusii vinavyoathiri kiimbo cha Kiswahili. Kutathmini jinsi usuli wa lugha na tajriba ya wanafunzi inavyochangia matumizi bora ya kiimbo katika uzungumzaji wa Kiswahili. Ili kuafiki madhumuni haya, maswali yafuatayo yalitumiwa: Je, wazungumzaji wa Ekegusii hufasili vipi kiimbo cha Kiswahili sanifu? Viarudhi vingine vya Ekegusii huathiri kiimbo cha Kiswahili vipi? Usuli na tajriba ya wanafunzi huchangia vipi katika matumizi bora ya kiimbo cha Kiswahili? Nadharia ya ujifunzaji wa kiimbo cha lugha ya pili iliyoasisiwa na Mennen (2015) ilitumiwa katika kuchunguza matumizi ya kiimbo. Utafiti huu ulifanywa maktabani na nyanjani. Maktabani ulihusu kusoma matini, vitabu, tasnifu, majarida na makala mtandaoni kuhusu kiimbo. Nyanjani ulijumuisha matumizi ya hojaji funge na wazi katika kupata tathmini ya wanafunzi ya sampuli ya data waliyopewa na mtafiti. Vilevile, mbinu ya mahojiano ambayo yalirekodiwa ilitumika kwa walimu wanaofunza Kiswahili. Pia, uchunzaji wa kushiriki ulitumiwa. Data ilichanganuliwa na kuwasilishwa kwa njia ya maelezo, majedwali, michoro na chati. Matokeo ya utafiti yalionyesha kuwa lugha ya Ekegusii huathiri matumizi ya kiimbo sahihi cha Kiswahili. Wazungumzaji wa Ekegusii walionyesha athari katika usomaji na ufasili wa kiimbo cha Kiswahili. Ilibainika kuwa viarudhi vingine vya Ekegusii huathiri matumizi ya kiimbo cha Kiswahili. Utafiti ulithibitisha kuwa jinsia huchangia katika matumizi sahihi ya kiimbo ambapo ilidhihirika kuwa jinsia ya kike hutumia kiimbo sahihi katika mazingira rasmi ikilinganishwa na jinsia ya kiume. Tajriba pia huchangia kiimbo sahihi pale ambapo wanafunzi ambao wamekuwa shuleni kwa muda mrefu huzungumza kwa kiimbo bora. Vifaa vya kisasa pia huchangia kuboresha matumizi ya kiimbo sahihi cha Kiswahili. Tunapendekeza walimu wakuze matumizi ya vifaa vya kisasa katika ufundishaji wa kiimbo cha Kiswahili, kuwepo sheria shuleni kuhusu matumizi ya Kiswahili katika mazingira rasmi na ufundishaji wa kiimbo utiliwe maanani kuanzia viwango vya chini vya elimu.
  • Item
    Tathmini ya Kiwango cha Ubadilishaji Msimbo Katika Vituo vya Moduli ya Masafa ya Mulembe na Moduli ya Masafa ya Sulwe
    (2023-11) Mabonga, Ivy; ; Peter Githinji
    Utafiti huu ulijikita katika kutathmini kiwango cha ubadilishaji msimbo katika vituo viwili vya Royal Media Services ambavyo ni vya moduli ya masafa ya Mulembe na Sulwe. Katika kituo cha Sulwe, lahaja ya Kibukusu imechukuwa nafasi ya lugha msingi huku lahaja za Kiluyia haswa Kikabrasi, Kiwanga, Kikhayo na lahaja zingine zikichukuwa nafasi ya lugha msingi katika kituo cha Mulembe . Ijapokuwa lugha hizo zinatumiwa katika mahojiano, matangazo na mambo mengine ya utangazaji wakati mwingine wageni na watangazaji hutumia Kiswahili. Kwa hivyo, utafiti huu uliangazia matumizi ya Kiswahili katika vituo hivyo ili kuweza kuchunguza kiwango chake katika ubadilishaji msimbo kupitia tathmini ya vichocheo vya ubadilishaji msimbo, ubainishaji wa jinsi ubadilishaji msimbo hutokea na uchanganuzi wa athari zinazotokana na ubadilishaji msimbo zinazojidhihirisha katika jamii hiyo. Kupitia malengo hayo, kiwango cha ubadilishaji msimbo kiliweza kutathminiwa kwa kuchunguza matumizi ya Kiswahili ambayo yalituwezesha kupima kiwango cha matumizi yake vituoni humo. Nadharia ya Maki iliyoasisiswa na Myers –Scotton (1993) ndio iliyoongoza utafiti huu. Nadharia hii ilijikita katika dhana za kutia na kutoa maki zilizowasilisha upya au ukawaida. Mkabala huu ulilinganisha lugha kadhaa ili kuangazia sababu zinazopelekea lugha moja kuchaguliwa kwa minajili ya matumizi miongoni mwa nyingine. Dhana ya kutia na kutoa maki hutumika katika nadharia hii kujenga msingi wa kubainisha vichocheo vya kisaikolojia na vya kijamii katika uchanganuzi wa msimbo. Mbali na hayo, nadharia hii inaeleza kuhusu maswala mengine kama vile ustadi au uwezo wa kuwasiliana, ambayo huchanganua maswala ya muktadha na ustadi.Mengine ni Haki na Majukumu ambayo hudhihirisha mazingira ya kutoa au kutia maki katika msimbo. Utafiti huu ulifanyika maktabani mno kwa kusoma tafiti na vitabu vilivyoandikwa kuhusu mada ambavyo vilikuwa nguzo ya utafiti huu. Utafiti wa nyanjani ulifanyika katika vituo teule kupitia usikilizaji wa baadhi ya vipindi na pia kuwahoji na wanahabari wa vituo hivyo. Data iliwasilishwa kwa njia ya kijarabati na kimaelezo, ili kuelezea na kuchanganua kikamilifu semi zenye ubadilishaji msimbo. Utafiti huu utawafaidi watafiti tathmini matumizi ya lugha katika jamii yenye wingi lugha iliyowekewa mipaka au huru. Kupitia ubainishaji wa athari ya Kiswahili kwa Kiluyia na vichocheo vilivyobainishwa, wanaisimu jamii wataweza kupima na kuchanganua mtagusano wa lugha kiidadi na kimaelezo.
  • Item
    Athari za Katama Mkangi kwa John Habwe: Mfano Kutoka kwa Riwaya Teule za Mafuta (1984) na Cheche za Moto (2008)
    (Kenyatta University, 2023-11) Musyoka, Kalingwa Felix; Titus M. Kaui
    Utafiti huu unashughulikia athari za Katama Mkangi kwa John Habwe kwa kujikita katika riwaya teule za Kiswahili za Mafuta (1984) na Cheche za Moto (2008). Utanzu wa riwaya ya Kiswahili umeendelea kupanuka kimaudhui na kifani kutokana na juhudi za watunzi mbalimbali kama vile Katama Mkangi na John Habwe. Japo tafiti za awali zimetafitia suala la mwingiliano matini, tafiti nyingi zimejikita katika kazi za mtunzi mmoja.Utafiti wa kina ulihitajika kuchunguza namna utunzi wa Mafuta (1984) ulivyoathiri John Habwe alipoitunga riwaya yake ya Cheche za Moto (2008). Katama Mkangi aliandika riwaya ya Mafuta katika wakati wa chama kimoja cha kisiasa ambapo uhuru wa kujieleza ulikuwa umebanwa sana. Habwe ameandika kazi yake ya Cheche za Moto katika mazingira yaleyale, miaka ishirini na minne baadaye. Wakati wa utunzi wa Cheche za Moto, uhuru wa kujieleza ulikuwa umepanuliwa. Kwa hivyo, amekwepa mtindo wa kimajazi alioutumia Mkangi na kuyaangazia masuala anayoyaibua Mkangi kwa njia wazi. Utafiti huu uliongozwa na malengo matatu: kwanza, ni kufafanua namna mwangwi wa maudhui ya riwaya ya Mafuta unavyojitokeza katika riwaya ya Cheche za Moto, kubainisha athari za usawiri wa wahusika wa Katama Mkangi kwa John Habwe, na mwisho, kuonyesha athari za kimtindo za Katama Mkangi kwa John Habwe. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya mwingiliano matini iliyoasisiwa na Julia Kristeva (1969). Mihimili mikuu ya nadharia hii iliyoongoza utafiti huu ni pamoja na: hakuna matini ya fasihi yenye sifa za pekee, matini hubainisha sifa mbalimbali za matini tangulizi, na mwisho, matini ya baadaye huweza kufafanua dhana fulani kutoka matini tangulizi kwa njia inayoeleweka. Nadharia hii ya mwingiliano matini ilisaidia pakubwa kuonyesha namna kazi ya awali, Mafuta (1984) ilivyomwathiri John Habwe katika utunzi wa Cheche za Moto (2008), kimaudhui na kifani. Riwaya ziliteuliwa kimakusudi ili kupata sampuli faafu yenye data ya kujaza pengo la utafiti. Data ilikusanywa kupitia kwa usomaji wa maktabani na vilevile kusakura mitandaoni kuhusu vipengele vya mwingiliano matini katika riwaya ya Kiswahili. Data hii imewasilishwa kwa njia ya kimaelezo. Utafiti huu unatarajiwa kutoa mchango katika uhakiki wa utanzu wa riwaya ya Kiswahili, hususan kuhusu kipengele cha kuathiriana baina ya watunzi wa riwaya za Kiswahili.
  • Item
    Uhusika katika vichwa vya habari za siasa kwenye gazeti la taifa leo (2017-2019)
    (Kenyatta University, 2021-12) Mutuku, Fidelis Kioko; Jacktone Onyango; Leonard Chacha
    Utafiti huu umechambua uhusika katika vichwa vya habari za siasa kwenye gazeti la Taifa Leo. Matoleo ya magazeti teule ya Taifa Leo yaliyochapishwa kati ya mwaka wa 2017 na 2019 yameongoza uchambuzi huu. Ili kufanikisha uchambuzi wa mantiki ya mada hii, nadharia ya uhusika inayoafiki malengo ya utafiti huu imetumikizwa. Malengo ya utafiti huu ni pamoja na; kudhihirisha na kuchambua dhana mbalimbali za uhusika katika vichwa vya habari za siasa kwenye gazeti la Taifa Leo, kutofautisha majukumu na maumbo ya uhusika katika vichwa vya habari husika na kubainisha umuhimu wa sarufi uhusika katika taaluma ya isimu. Uhusika ni kategoria ya kisarufi ambayo huonyesha uhusiano wa viambajengo katika tungo. Aidha, uamilifu wa kila kiambajengo katika tungo na athari ya kila kiambajengo kwa viambajengo vingine huonyeshwa. Nyenzo ya data msingi ya utafiti huu ni maktaba. Mbinu ya upekuzi wa yaliyomo ilitumika katika ukusanyaji wa data hii, ambapo machapisho mbalimbali ya gazeti la Taifa Leo (2017-2019) yanayotawaliwa na kigezo cha siasa yalipitiwa na mtafiti kwa umakinifu kabla ya kufanywa data teule. Katika uwasilishi wa data, maelezo yameandamana na michoroti ya kisintaksia pamoja na majedwali. Kijumla, mpangilio wa kazi hii umewasilishwa kwenye sura tano. Sura ya kwanza ni utangulizi wa utafiti ulioshughulikia suala la utafiti, malengo ya utafiti, upeo na mipaka ya utafiti, misingi ya nadharia na mbinu za utafiti. Katika sura ya pili, mtafiti amebaini kuwa, miundo mbalimbali ya vichwa vya habari za siasa zina aina zifuatazo za uhusika; uhusika kiima, mahali, yambwa, tendea, tokeo na ala. Vichwa hivi vya habari huwa na kategoria mbili za uwakilisho, nazo ni; muundo ndani na muundo nje. Kwenye sura ya tatu, mtafiti ameweka wazi tofauti iliyoko kati ya majukumu na maumbo ya uhusika. Mtafiti amebainisha kuwa, majukumu ya uhusika ni dhahania ilhali maumbo yake huonekana. Umuhimu mbalimbali wa sarufi uhusika katika taaluma ya isimu umeelezwa ipasavyo katika sura ya nne. Baadhi ya umuhimu huo ni kurahisisha uelewaji wa sentensi katika lugha, kutambua dhima ya maneno katika tungo na kadhalika. Hatimaye sura ya tano imeangazia matokeo, changamoto na mapendekezo ya utafiti. Mtafiti ameeleza matokeo ya utafiti huu kama ifuatavyo; Kiswahili hakina maumbo dhahiri ya uhusika isipokuwa viwakilishi vya nafsi ya pili na tatu, umoja na wingi. Hata hivyo, vichwa vya habari ambavyo muundo wake hauruhusu uwepo wa viwakilishi hivi, viwakilishi ....
  • Item
    Tathmini ya Kiwango cha Ubadilishaji Msimbo katika Vituo vya Moduli ya Masafa ya Mulembe na Moduli ya Masafa ya Sulwe
    (Kenyatta University, 2023) Mabonga, Ivy; Peter Githinji
    Utafiti huu ulijikita katika kutathmini kiwango cha ubadilishaji msimbo katika vituo viwili vya Royal Media Services ambavyo ni vya moduli ya masafa ya Mulembe na Sulwe. Katika kituo cha Sulwe, lahaja ya Lubukusu imechukuwa nafasi ya lugha msingi huku lahaja za Kiluhya haswa Lukabrasi, Luwanga, Lukhayo na lahaja zingine zikichukuwa nafasi ya lugha msingi katika kituo cha Mulembe. Ijapokuwa lugha hizo zinatumiwa katika mahojiano, matangazo na mambo mengine ya utangazaji wakati mwingine wageni na watangazaji hutumia Kiswahili. Kwa hivyo, utafiti huu uliangazia matumizi ya Kiswahili katika vituo hivyo ili kuweza kutathmini kiwango chake katika ubadilishaji msimbo kupitia tathmini ya vichocheo vya ubadilishaji msimbo, ubainishaji wa jinsi ubadilishaji msimbo hutokea na uchanganuzi wa athari zinazotokana na ubadilishaji msimbo zinazojidhihirisha katika jamii hiyo. Kupitia malengo hayo, kiwango cha ubadilishaji msimbo kiliweza kutathminiwa kwa kuchunguza matumizi ya Kiswahili ambayo yalituwezesha kupima kiwango cha matumizi yake vituoni humo.Nadharia ya Maki iliyoasisiswa na Myers –Scotton (1993) ndio iliyoongoza utafiti huu. Nadharia hii ilijikita katika dhana za kutia na kutoa maki zilizowasilisha upya au ukawaida. Mkabala huu ulilinganisha lugha kadhaa ili kuangazia sababu zinazopelekea lugha moja kuchaguliwa kwa minajili ya matumizi miongoni mwa nyingine. Dhana ya kutia na kutoa maki hutumika katika nadharia hii kujenga msingi wa kubainisha vichocheo vya kisaikolojia na vya kijamii katika kuchanganuzi wa msimbo. Mbali na hayo, nadharia hii inaelezea maswala mengine kama vile ustadi au uwezo wa kuwasiliana, ambayo huchanganua maswala ya muktadha na ustadi.Mengine ni haki na majukumu ambayo hudhihirisha mazingira ya kutoa au kutia maki katika msimbo. Utafiti huu ulifanyika maktabani mno kwa kusoma tafiti na vitabu vilivyoandikwa kuhusu mada ambavyo vilikuwa nguzo ya utafiti huu. Utafiti wa nyanjani ulifanyika katika vituo teule kupitia usikilizaji wa baadhi ya vipindi na mahojiano na wanahabari wa vituo hivyo. Data iliwasilishwa kwa njia ya kijarabati na kimaelezo, ili kuelezea na kuchanganua kikamilifu semi zenye ubadilishaji msimbo. Utafiti huu utawafaidi watafiti tathmini ya matumizi ya lugha katika jamii yenye wingi lugha iliyowekewa mipaka au huru. Kupitia ubainishaji wa athari ya Kiswahili kwa Kiluhya na vichocheo vilivyobainishwa, wanaisimu jamii wataweza kupima na kuchanganua mtagusano wa lugha kiidadi na kimaelezo.
  • Item
    Utata kama Chanzo cha Taharuki Katika Vichwa vya Habari Katika Gazeti la Taifa Leo
    (Kenyatta University, 2023) Njeru, Joyce Wanjiru; leonard chacha mwita
    Utafiti huu ulidhamiria kutathmini utata kama chanzo cha taharuki katika vichwa vya habari katika gazeti la Taifa Leo. Pia, utafiti huu ulilenga kuweka wazi athari ya utata uliopo katika vichwa vya habari kwa wasomaji wa gazeti la Taifa Leo. Gazeti ni njia mwafaka na muhimu ya kuwasilisha ujumbe kama vile masuala nyeti, sera za serikali, masuala ibuka na ujumbe mwingine wowote. Wasomaji ndio wapokezi wa habari hizo. Hivyo, ni muhimu kuchunguza athari ya utata huo kwa wasomaji kwani ndio walengwa. Nia ya wahariri wa gazeti ni kupitisha ujumbe. Vichwa vya habari ni sehemu muhimu ya kuwapa wasomaji msukumo wa kusoma habari zilizopo katika gazeti na hivyo, vichwa vinapaswa kuibua taharuki ili kuvutia wasomaji wasome ujumbe huo. Hivyo basi, utafiti huu ulilenga kuchunguza iwapo vichwa vya habari vyenye utata vinaibua taharuki katika gazeti la Taifa Leo. Taharuki ilichukuliwa kuwa, hamu ya kutaka kujua yanayofafanuliwa katika habari baada ya kusoma kichwa fulani cha habari, yaani msukumo ambao huchochea wasomaji kutaka kujua kinachozungumziwa katika habari inayofuata. Pia, utafiti huu uliweza kuweka bayana maoni ya wasomaji wa gazeti la Taifa Leo kuhusiana na utata katika vichwa vya habari. Nadharia iliyotumiwa katika utafiti huu ni nadharia ya maana kama matumizi iliyoasisiwa na Wittgenstein mwaka wa 1930 ambayo ilituelekeza kuchunguza maana ya maneno katika muktadha wa mutumizi yake. Utafiti huu ulifanywa maktabani na nyanjani. Maktabani, mtafiti alisoma vitabu na majarida yaliyo jadili kuhusu utata na kuchambua vichwa vya habari vyenye utata katika gazeti la Taifa Leo ili kubainisha aina mbalimbali za utata. Utata uliobainika katika data iliyokusanywa ni utata wa kileksia, utata wa kimantiki, utata wa kutafakari, utata wa kipragmantiki na utata wa kisarufi. Nyanjani, wasomaji, wahariri na waandishi wa gazeti la Taifa Leo walihojiwa ili kutathmini athari ya utata uliopo katika vichwa vya habari na iwapo utata huo huzua taharuki kwa wasomaji. Matokeo ya utafiti huu yalidhihirisha kuwa asilimia kubwa ya wasomaji huwa na athari chanya kuhusu utata katika vichwa vya habari na vichwa hivyo huzua taharuki kwa wengi wa wasomaji wa gazeti la Taifa Leo. Hata hivyo, ilibainika kuwa wakati mwingine utata uchanganya na kupotosha ujumbe lengwa na hivyo kutozua taharuki kwa wasomaji. Hivyo, wahariri wanapaswa kuwa makini wanapoteua vichwa vya habari ili vizue taharuki. Utafiti huu utawasaidia waandishi na wahariri wa gazeti kutambua athari na maoni ya wasomaji kuhusiana na vichwa vya habari vyenye utata na mchango wa utata katika kuzua taharuki. Hili litawasaidia kuwasilisha ujumbe ipasavyo wakitilia maanani wasomaji wa gazeti. Pia, utafiti huu utapanua fikra za wasomaji kuhusu utata katika vichwa vya habari kwa kuwa uliweza kuchambua utata kwa kina.