Tathmini ya Kiwango cha Ubadilishaji Msimbo Katika Vituo vya Moduli ya Masafa ya Mulembe na Moduli ya Masafa ya Sulwe

Loading...
Thumbnail Image
Date
2023-11
Authors
Mabonga, Ivy
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Abstract
Utafiti huu ulijikita katika kutathmini kiwango cha ubadilishaji msimbo katika vituo viwili vya Royal Media Services ambavyo ni vya moduli ya masafa ya Mulembe na Sulwe. Katika kituo cha Sulwe, lahaja ya Kibukusu imechukuwa nafasi ya lugha msingi huku lahaja za Kiluyia haswa Kikabrasi, Kiwanga, Kikhayo na lahaja zingine zikichukuwa nafasi ya lugha msingi katika kituo cha Mulembe . Ijapokuwa lugha hizo zinatumiwa katika mahojiano, matangazo na mambo mengine ya utangazaji wakati mwingine wageni na watangazaji hutumia Kiswahili. Kwa hivyo, utafiti huu uliangazia matumizi ya Kiswahili katika vituo hivyo ili kuweza kuchunguza kiwango chake katika ubadilishaji msimbo kupitia tathmini ya vichocheo vya ubadilishaji msimbo, ubainishaji wa jinsi ubadilishaji msimbo hutokea na uchanganuzi wa athari zinazotokana na ubadilishaji msimbo zinazojidhihirisha katika jamii hiyo. Kupitia malengo hayo, kiwango cha ubadilishaji msimbo kiliweza kutathminiwa kwa kuchunguza matumizi ya Kiswahili ambayo yalituwezesha kupima kiwango cha matumizi yake vituoni humo. Nadharia ya Maki iliyoasisiswa na Myers –Scotton (1993) ndio iliyoongoza utafiti huu. Nadharia hii ilijikita katika dhana za kutia na kutoa maki zilizowasilisha upya au ukawaida. Mkabala huu ulilinganisha lugha kadhaa ili kuangazia sababu zinazopelekea lugha moja kuchaguliwa kwa minajili ya matumizi miongoni mwa nyingine. Dhana ya kutia na kutoa maki hutumika katika nadharia hii kujenga msingi wa kubainisha vichocheo vya kisaikolojia na vya kijamii katika uchanganuzi wa msimbo. Mbali na hayo, nadharia hii inaeleza kuhusu maswala mengine kama vile ustadi au uwezo wa kuwasiliana, ambayo huchanganua maswala ya muktadha na ustadi.Mengine ni Haki na Majukumu ambayo hudhihirisha mazingira ya kutoa au kutia maki katika msimbo. Utafiti huu ulifanyika maktabani mno kwa kusoma tafiti na vitabu vilivyoandikwa kuhusu mada ambavyo vilikuwa nguzo ya utafiti huu. Utafiti wa nyanjani ulifanyika katika vituo teule kupitia usikilizaji wa baadhi ya vipindi na pia kuwahoji na wanahabari wa vituo hivyo. Data iliwasilishwa kwa njia ya kijarabati na kimaelezo, ili kuelezea na kuchanganua kikamilifu semi zenye ubadilishaji msimbo. Utafiti huu utawafaidi watafiti tathmini matumizi ya lugha katika jamii yenye wingi lugha iliyowekewa mipaka au huru. Kupitia ubainishaji wa athari ya Kiswahili kwa Kiluyia na vichocheo vilivyobainishwa, wanaisimu jamii wataweza kupima na kuchanganua mtagusano wa lugha kiidadi na kimaelezo.
Description
Tasnifu Hii Imewasilishwa Kwa Idara Ya Kiswahili ili Kutosheleza Baadhi ya Mahitaji ya Shahada ya Uzamili Katika Chuo Kikuu Cha Kenyatta, Novemba, 2023
Keywords
Tathmini, Kiwango, Ubadilishaji, Msimbo, Vituo, Moduli, Masafa, Mulembe, Moduli, Masafa, Sulwe
Citation