MST-Department of Kiswahili and African Languages
Permanent URI for this collection
Browse
Recent Submissions
Item Wakaa, Uwasilishaji Usemi na Wahusika katika Hotuba Teule za Wanasiasa wa Kenya(Kenyatta University, 2025-11) Mukonambi, Kekonen Stanley; King'ei, Kitula Osore, MiriamUtafiti huu ulichunguza wakaa, uwasilishaji usemi na wahusika katika hotuba teule za wanasiasa wa Kenya. Baadhi ya wanasiasa hutumia hotuba zinazovuta makini ya wasikilizaji na wafuasi wao kwa mitindo tofauti. Mojawapo ya mbinu hizi za kimtindo ni usimulizi. Utafiti huu ulichunguza vipengele vya usimulizi; wakaa, uwasilishaji wa usemi na wahusika. Wakaa ni mpangilio wa matukio katika hadithi. Uwasilishaji wa usemi ni namna ambavyo maana hutolewa kwa kutumia lugha ilhali wahusika ni viumbe wa kisanaa wanaoendeleza kazi ya kifasihi. Malengo ya utafiti huu ni: kubainisha vipengee vya wakaa, uwasilishaji wa usemi na wahusika katika hotuba teule na kujadili dhima ya wakaa, uwasilishaji usemi na wahusika katika hotuba teule. Nadharia iliyotumika ni ya Naratolojia kwa kuzingatia mawazo yake Rimmon-Kenan. Mtazamo wake ni wazi kwani huwasaidia wasomaji kutofautisha kwa urahisi viwango vya masimulizi na kuchanganua matini kwa hatua. Aidha, haujatumika na tafiti nyingi ikilinganishwa na ule wa Gerald Genette. Mihimili yake ilifaa kwani iliweka wazi vipengele ambavyo vilishughulikiwa na kutathmini nafasi yavyo katika uelewekaji wa hotuba teule. Uteuzi wa sampuli kimaksudi ulitumika kuteua hotuba teule za Rais mstaafu Uhuru Kenyatta wa chama cha TNA na JP, Mhes. Raila Odinga wa chama cha ODM na Rais Dkt. William Ruto wa chama cha URP, JP na UDA zilizotolewa kati ya mwaka 2013 hadi 2023. Utafiti ulifanyika maktabani ambako data ilikusanywa kwa njia za usomaji makini kwa kupitia makala, nyaraka, majarida, tasnifu za awali na kutazama na kusikiza makala ya mtandao wa YouTube. Ufafanuzi wa kimaelezo kwa kuzingatia nadharia ulitumiwa kutolea matokeo ya utafiti ambayo yamewasilishwa kwenye vijimada vilivyomo katika sura tano za tasnifu hii. Matokeo ya utafiti huu yanatoa mchango katika taaluma ya fasihi kwa wahakiki na wanafunzi kufahamu nafasi ya vipengee hivi katika hotuba. Aidha, unawafaidi wahakiki na watafiti wa fasihi kwa kuwaelekeza jinsi ya kuhakiki hotuba.Item Tathmini ya Sura za Ufisadi Katika Riwaya za Tom Olali Mafamba (2012) na Watu wa Gehenna (2012)(Kenyatta University, 2025-11) Musyoki, Pauline Kamanthe; King'ei, Kitula Osore, MiriamUtafiti huu unafafanua sura tofauti za ufisadi. Mtafiti amefanya hivi kwa kushughulikia riwaya ya Mafamba (Olali, 2012) na Watu Wa Gehenna (Olali, 2012). Ufisadi ni suala tata ulimwenguni na hata nchini Kenya. Dhana hii ni pana ila maelezo yake katika fasihi ni finyu kwa kuwa, msisitizo umekuwa kwenye matumizi ya fedha za umma.Kulingana na Tume ya EACC (2016) kipengele cha iv, ufisadi unahusu unyanyasaji katika ofisi za umma, upendeleo, hongo, ulaghai, ukosefu wa uaminifu katika ofisi za umma, kutolipa ushuru au ada yoyote ile na kutofuata sheria zilizohidhinishwa kuteua viongozi katika ofisi za umma. Mtafiti ameangazia masuala hayo kwa kutathmini riwaya teule kwa lengo la kubainisha namna masuala hayo yalivyosawiriwa na kuleta uwezekano wa sura tofauti za ufisadi. Wahakiki kama vile; Muthumbi (2005), Ochenja (2008), Mayieka (2015), Sereti (2016), Mwaniki (2018) na wengineo wameeleza ufisadi kama matumizi mabaya ya fedha za umma na ndio sababu utafiti huu umeangazia sura tofauti za ufisadi. Riwaya zimeteuliwa kimakusudi na zimeangazia sura tofauti za ufisadi hivyo zilitupa data mwafaka. Nadharia ya Uhalisia wa Kijamaa na Udenguzi zilitumika. Nadharia ya Uhalisia wa Kijamaa inahusishwa na Karl Marx na fikra zake zilitokana na zile za mwanafalsafa Hegel (1971). Waitifaki wake ni Gorky, Baxandall, Terry, James Bisztray na wengine.Kumekuwa na ufisadi katika jamii yoyote ya kitabaka tangu Ujima,Utumwa ,Umwinyi, Ubepari, Ujamaa na Ukumiunisti. Nadharia hii hivyo basi ilitumika kuangazia mfumo wa kiuchumi ambapo kuna tabaka la juu na chini. Tabaka la juu huwa na mifumo ya uzalishaji mali. Njia wanazotumia kumiliki mali ni ufisadi. Tabaka la juu hukiuka maadili ya kiutawala wakijinufaisha na kudhalilisha watu wa tabaka la chini. Kwa kuwa nadharia hii inaelezea uhalisia kama ulivyo, haikuwezesha kutafuta maana zinginezo za ufisadi hivyo nadharia ya Udenguzi ilimfaa mtafiti kuangazia fasiri mbalimbali za ufisadi. Nadharia ya Udenguzi iliasisiwa na Jacques Derrida (1962).Waitifaki wake ni pamoja na Foucault, Roland Barthes, Jean Baudrillard Paul de Man, J.Hillis Miller, Jacques Lacan, Barbara Johnstone na wengineo. Kupitia mihimili ya nadharia hii mtafiti alieleza fasiri mbalimbali za ufisadi. Utafiti huu ulifanywa maktabani kwa kusoma vitabu teule, tasnifu, majarida na makala ya mitandaoni yanayohusiana na mada. Data ya kimsingi ilitolewa kwenye riwaya teule. Data hiyo ilichanganuliwa kwa kuzingatia malengo na nadharia zinazoongoza utafiti. Matokeo yamewasilishwa kwa kutumia njia ya maelezo. Utafiti huu utakuwa muhimu kwa wasomi na jamii kwa jumla hasa kwa kuagazia suala tata la ufisadiItem Tathmini ya Uainishaji wa Tanzu na Vijitanzu vya Fasihi Simulizi katika Vitabu Vilivyoidhinishwa: Kaunti ya Makueni(Kenyatta University, 2025-10) Munyao, Carolyne NzilaniUtafiti huu unahusu tathmini ya uainishaji wa tanzu na vijitanzu vya fasihi simulizi katika vitabu vilivyoteuliwa kufunza fasihi simulizi ya Kiswahili kwa walimu na wanafunzi katika Shule za Upili Kenya, Kaunti ya Makueni. Utafiti ulilenga kuonyesha ukinzano wa idadi ya tanzu na vijitanzu na matatizo yanayokumba wanafunzi na walimu katika uainishaji wa fasihi simulizi. Masuala matatu yalilengwa katika utafiti huu: kubainisha tofauti katika uainishaji wa tanzu na vijitanzu vya fasihi simulizi katika vitabu vilivyoidhinishwa, kubainisha vigezo vilivyotumiwa na kupendekeza suluhisho kwa utata unaotokana na tofauti hizi za uainishaji. Nadharia mbili zilitumiwa:ya Tanzu na ya Ujifunzaji na Upokeaji wa Lugha ya Pili (Second Language Learning and Acquisition) iliyoasisiwa na Krashen (1982) ambapo haipothesia ya mchakato (Input hypothesis) zilitumiwa kufanikisha malengo ya utafiti huu. Haipothesia hii ilihusu sheria katika upokezi wa lugha, kusonga kutoka kwa dhana rahisi hadi ngumu na uelewa wa maarifa kutoka (i+1) ambapo i ni maarifa yaliyopo tayari na 1 ni maarifa yanayopatikana baadaye kupitia ujifunzaji. Nadharia ya Tanzu ilijikita kwa maswali je, tanzu zipo? Je, kuna idadi mahsusi ya tanzu? na Je, tanzu zinajisimamia au zinaingiliana? Nadharia hii ililenga uainishaji wa tanzu na vigezo vya uainishaji. Uteuzi wa kimakusudi ulitumiwa kuteua vitabu vilivyoidhinishwa na taasisi ya kukuza mitaala vya kufundishia fasihi simulizi kwa shule za upili, vitabu hivi viliwapa watafiti data ya kimsingi (maktabani) ilhali data endelezi (nyanjani) ilitokana na wanafunzi na walimu. Shule nne za upili ziliteuliwa ambapo wanafunzi ishirini wa kidato cha nne walihojiwa. Aidha, walimu wawili wa Kiswahili katika kila shule waliteuliwa na kuhojiwa. Muundo wa utafiti huu ni wa kimaelezo. Data iliyopatikana ilichanganuliwa kwa mtindo wa kimaelezo na kuwasilishwa kwa maelezo fafanuzi na majedwali. Matokeo ya utafiti huu yalibainisha kuwa vitabu tofauti vilivyoidhinishwa kufundishia fasihi simulizi kwa shule za upili vilikuwa na uainishaji unaotofautiana wa tanzu na vijitanzu vya fasihi simulizi. Baadhi ya vitabu vina tanzu nne, vingine tano na vingine sita. Pamoja na hayo, utafiti ulibaini kuwa uainishaji wa tanzu na vijitanzu vya fasihi simulizi unategemea vigezo na misingi mbalimbali inayofuatwa na wataalamu katika kuandika matini za fasihi simulizi kama vile; muundo, maudhui, wakati, mtindo, wahusika na kadhalika. Ilibainika kuwa, ni kwa sababu hii kunatokea utata katika vitabu vilivyoidhinishwa. Kwa mujibu wa nadharia ya Ujifunzaji na Upokeaji wa Lugha ya Pili, iwapo mada zitawasilishwa kwenye vifaa kwa njia isiyo wazi basi kutakuwa na changamoto kwa wasomaji. Aidha, kupitia hojaji, wasailiwa walikiri kuwa kuna utata katika ufundishaji na usomaji wa fasihi simulizi kutokana na hali hii. Hivyo basi, mtafiti alipendekeza kuwa, mada za fasihi simulizi zinastahili kuratibiwa upya ili ziwafae wanafunzi na walimu katika shule za upili. Utafiti huu ni wa manufaa kwa watafiti, wahakiki, waandishi wa vitabu vya fasihi simulizi, walimu na wanafunzi wa Shule za Upili na waratibu wa mitaala.Item Mielekeo ya Wauza Mifugo Mnadani Wanaozungumza Kinandi Kuhusu Kiswahilikatika Kaunti ya Nandi(Kenyatta University, 2025-11) Jepkemboi ,Anne; King'ei, Kitula Osore, MiriamUtafiti huu ulilenga kueleza jinsi mielekeo ya wauza mifugo mnadani katika kaunti ya Nandi kuhusu lugha ya Kiswahili inavyoathiri matumizi yao ya lugha. Mwelekeo wa watu kuhusu vitu au dhana unaweza kuathiri wale watu au dhana hizo. Tafiti tofauti zilizofanywa kuhusu mielekeo ya watu kwa lugha zimebaini kuwa mielekeo ya watu huweza kuwa hasi au chanya kutegemea masiala mbalimbali kama vile elimu, umri, mazingira, jinsia na kadhalika. Utafiti huu uliongozwa na malengo yafuatayo: kupambanua mielekeo ya wauza mifugo mnadani wanaozungumza Kinandi kwa lugha ya Kiswahili katika kaunti ya Nandi; kubainisha mambo ambayo husababisha mielekeo ya wauza mifugo mnadani wanaozungumza Kinandi kuhusu lugha ya Kiswahili na kuchunguza athari ya mielekeo hiyo ya lugha kwa maendeleo ya Kiswahili katika jamii hii. Nadharia ya Utendaji Razini (Theory of Reasoned Action) iliyoasisiwa na Fishbein na Ajzen (1975) ilitumiwa kuongoza utafiti huu. Wataalamu hawa wanasema kuwa binadamu ni viumbe wanaofikiria na wanajua aina ya mielekeo na tabia walizo nazo. Kwa hivyo, maelezo ya watafiti hawa yanalingana na lengo la utafiti huu ambalo ni kueleza matumizi ya Kiswahili miongoni mwa wauza mifugo mnadani ambao mielekeo yao hudhihirika kupitia matumizi yao ya lugha. Utafiti huu ulihusisha wauza mifugo 35 kutoka minada yote 7 katika kaunti ya Nandi. Mtafiti alitumia idadi hii kimaksudi. Utafiti huu ulitumia mbinu ya utafiti wa maelezo ambapo data ilikusanywa kupitia hojaji, mahojiano na kushiriki utendaji kisha ikachanganuliwa na kuwasilishwa kupitia majedwali, baa grafu na pai chati. Ilibainika kwamba wauza mifugo mnadani wana mitazamo hasi kuhusu utumiaji wa Kiswahili kwa sababu wanahisi Kiswahili ni kigumu kwao. Matokeo ya utafiti huu yanaweza kutumiwa na washikadau mbalimbali wanaohusika na lugha ili kuweka mikakati ya kuhakikisha kuwa Wakenya wote wanafahamu na kutumia kwa ufasaha lugha ya Kiswahili ili wabadili mielekeo yao hasi kuhusu lugha hii.Item Maudhui ya Ukungwi katika Nyimbo Teule za Taarab(Kenyatta University, 2025-11) Wendo, Fadhili HamisiUtafiti huu umechunguza jinsi maudhui ya ukungwi yanavyojitokeza katika nyimbo teule za taarab. Malengo yafuatayo yalinuiwa kutekelezwa; kubainisha dhima ya kungwi katika jamii ya Waswahili, kuchunguza maudhui ya ukungwi katika nyimbo teule za taarab na kulinganisha dhima ya kungwi na maudhui ya ukungwi katika nyimbo teule za taarab. Sampuli iliteuliwa kimaksudi ambapo kati ya nyimbo nyingi za taarab, nne ndizo ziliteuliwa kutumika katika utafiti huu. Nyimbo hizi ni: Maji ya Uvuguvugu (Wachonga Vinyago), Nenda salama (Omar Kopa), Ndoa (Aslay na Khadija Kopa), Bi Harusi (AT). Sampuli ya utafiti huu iliteuliwa kwa kutumia mbinu ya kimakusudi. Kati ya maeneo mengi katika jamii ya Waswahili, eneo la Msambweni ndilo lililoteuliwa kutumika katika utafiti. Mbinu hii ilifaa katika kuwateua makungwi waliochangia data muhimu ya kuchanganuliwa. Utafiti huu uliongozwa na nadharia mbili; nadharia ya Simiotiki na nadharia ya Uamilifu. Nadharia ya Simiotiki iliasisiwa na Ferdinand Dessaussure (1913) na Charles Pierce (1977) na inahusu uhusiano uliopo kati ya kitaja na kitajwa na matumizi ya ishara, picha na msimbo. Nadharia hii ilisaidia katika kufafanua mbinu za uwasilishaji wa ujumbe katika nyimbo teule za taarab. Kwa upande mwingine nadharia ya Uamilifu iliasisiwa na Emile Dukheim (1912) na inahusika na uchambuzi wa dhima zinazojitokeza katika kazi za fasihi. Hii ilituongoza katika kubainisha dhima ya kungwi katika jamii. Utafiti huu ulikuwa wa kimaktaba na wa nyanjani ambapo maktabani; mtafiti aliweza kusoma tasnifu, makala na majarida yanayohusiana na mada. Nyanjani, mtafiti alitembelea eneo lengwa ili kuwahoji baadhi ya makungwi kuhusu dhima yao. Matokeo yalionyesha kuwa kungwi ana jukumu la kuwafundisha wanawali kuhusu maswala ya unyumba yakiwemo usafi wa mwili na nyumba, namna ya kumhudumia mume, namna ya kusema na marafiki na jamaa za mume, matumizi ya vifaa vya kiasili kama vile mbuzi, kinu, mchi ufagio miongoni mwa mengine. Aidha, maudhui haya ya ukungwi yanafundishwa na waimbaji wa nyimbo teule za taarab na kuonyesha namna kipera cha nyimbo na mawaidha vinaingiliana kimaudhui. Utafiti huu unatarajiwa kutoa mchango wa kuonyesha jinsi vitanzu vya mawaidha na nyimbo huingiliana kidhima.Item Mtazamo Linganishi WA Itikadi Katika Utenzi WA Mwanakupona na Mashairi Ya Muyaka(Kenyatta University, 2025-11) Mutembei, Doreen NkathaUtafiti huu ulilenga kulinganisha itikadi katika mashairi ya Muyaka na Utenzi wa Mwanakupona. Dhana ya itikadi ni dhana changamano na pana na imeibua mijadala mingi baina ya wataalamu mbalimbali. Itikadi ni muhimu kwa sababu huelekeza matendo yote ya mtunzi kuhusu yale atakayowasilisha na namna atakavyowasilisha kazi yake. Kwa hivyo, itikadi ndio huongoza misimamo, mielekeo na imani ya mtunzi. Vitabu teule vya kufanikisha utafiti huu ni mashairi ya Muyaka na Utenzi wa Mwanakupona. Vitabu hivi viliteuliwa kwani ingawa kazi hizi ziliandikwa katika kipindi kimoja, ni tofauti kimtindo na kimaudhui. Hivi ni kusema kuwa watunzi hawa waliongozwa na itikadi tofauti. Kwa hivyo, ni muhimu kuchunguza na kuzilinganisha zile itikadi katika mashairi ya Muyaka na Utenzi wa Mwanakupona na jinsi itikadi husika zinazowaongoza watunzi hao zinavyolingana na kujitokeza katika kazi zao. Utafiti huu uliongozwa na malengo yafuatayo: kubaini itikadi katika Utenzi wa Mwanakupona na mashairi ya Muyaka, kutathmini jinsi athari za itikadi zinavyopelekea uwasilishaji wa maudhui kwenye Utenzi wa Mwanakupona na mashairi ya Muyaka na kuchunguza athari za itikadi katika uwasilishaji wa mtindo katika mashairi ya Muyaka na Utenzi wa Mwanakupona. Nadharia ya itikadi, mikabala ya Karl Marx (1977 na 1979), Louis Althusser (1981) na Antonio Gramsci (1985) ilitumika. Mkabala wa Karl Marx umetumika kwani unashikilia kuwa itikadi ni ‘ungamuzi potoshi.’ Mkabala wake Louis Althusser umetumika kwani aliorodhesha vyombo vya kiitikadi ambavyo alivigawa katika vikundi viwili. Vinavyo endeleza itikadi moja kwa moja kama vile polisi, jeshi, mahakama na serikali. Pia, vyombo visivyo vya moja kwa moja kama dini, elimu, vyombo vya habari na familia. Mwisho, mkabala wake Antonio Gramsci umetumika kwani Gramsci anaieleza dhana hii ya itikadi kama fikra, mitazamo na mielekeo ambayo binadamu huchukulia kuwa za kawaida hivyo kujikandamiza kwa hiari yake mwenyewe. Data husika ilitolewa maktabani ambapo shairi, beti, mishororo na vipande vya mishororo vilivyo na dhana za kiitikadi zilikusanywa. Mbinu ya usampulishaji wa kimaksudi ilitumika katika uteuzi wa sampuli. Data ilichanganuliwa na kuwasilishwa kwa njia ya kimaelezo ili iweze kueleweka. Kutokana na data ya utafiti huu, imebainika kuwa Muyaka na Mwanakupona waliongozwa na itikadi tofauti ingawa walikuwa watunzi wa kipindi kimoja cha kirasimi. Itikadi hizo zilipelekea uwasilishaji wao wa maudhui na mtindo vitofauti.Item Majazi na Stiari katika Riwaya ya Dunia Yao na Nyuso za Mwanamke(Kenyatta University, 2024-12) Mathuku, JosephUtafiti huu ulichunguza matumizi ya majazi na stiari katika riwaya mbili teule za Said Ahmed Mohamed nazo ni Dunia Yao (2006) na Nyuso za Mwanamke (2010). Utafiti huu ulilenga kubaini majazi na stiari katika kazi teule, nafasi ya majazi na stiari katika kuwasawiri wahusika na kuonyesha jinsi mtunzi ametumia tamathali hizi kuibua maudhui. Utafiti huu ulikuwa wa kimaelezo na wa maktabani. Uteuzi wa sampuli ulikuwa wa kimakusudi ukilenga riwaya za Said Ahmed Mohamed nazo ni Dunia Yao (2006) na Nyuso za Mwanamke (2010). Ukusanyaji wa data ulihusisha usomaji wa kina wa riwaya teule ili kupata data inayokusudiwa. Hizi ni riwaya ambazo zimesheheni matumizi ya majazi na stiari. Data ilichanganuliwa kwa kuongozwa na malengo ya utafiti pamoja na mihimili ya nadharia ya Mtindo na ile ya Matumizi ya Stiari. Nadharia ya Mtindo inashikilia kuwa kazi za kifasihi haziwezi kuibuliwa bila matumizi ya lugha nayo nadharia ya Matumizi ya Stiari hushikilia kuwa ili kuelewa dhana moja ya kistiari yafaa tuilinganishe na nyingine iliyo na sifa zile zile zinazorejelewa. Uwasilishaji wa data hiyo ulikuwa wa kimaelezo. Riwaya ya Dunia Yao (2006) na ile ya Nyuso za Mwanamke (2010) tulizozitafitia ziliandikwa mwanzo mwanzo wa Karne ya 21 na zilidhihirisha mkondo mpya wa kutunga kazi za kifasihi (ule wa usasa baadaye). Riwaya hizi zilisheheni matumizi mapya na ya kipekee ya majazi na stiari ambapo uwasilishaji wa uhalisia na usawiri wa wahusika sasa haufanywi kwa kufuata mkondo wa hurafa kama hapo awali bali unahusisha matumizi mapya ya majazi na stiari ambapo hadithi, wahusika, matukio na mandhari huweza kufasiriwa au kusomwa ili ziweze kuleta zaidi ya kiwango kimoja cha maana. Utafiti huu utawafaa wahakiki wa riwaya ya Kiswahili, wasomi na watunzi wa kazi za kifasihi kuona namna waandishi wa tungo za kifasihi wa Karne hii ya 21 wanavyotumia tamathali za usemi kwa njia ya kipekee kuwasilisha uhalisia.Item Uchanganuzi Linganishi wa Matini ya Hotuba za Kisiasa Kuhusu Ufisadi Kuanzia Mwaka 2015 Hadi 2020(Kenyatta University, 2025-06) Mworeh, Felix Shimenga; King'ei, Kitula Osore, MiriamHotuba ni chombo muhimu kinachotumiwa na wanasiasa kuwasilisha sera zao, itikadi na hata kukemea maovu yanayotendeka katika jamii. Nchini Kenya, suala la ufisadi ni mojawapo ya maovu yanayotekelezwa na baadhi ya viongozi na wananchi. Kwa sababu hii, wanasiasa wengi huliangazia suala hili katika hotuba zao kwa umma kama mojawapo ya mikakati ya kuupiga vita ufisadi. Wao hutumia lugha kwa njia ya kipekee wanapoangazia suala hili hususan vita dhidi yake. Hii basi ndiyo sababu utafiti huu ulilenga kuchanganua na kulinganisha matini ya hotuba za kisiasa zinazoangazia suala la ufisadi nchini Kenya. Utafiti uliongozwa na nadharia ya Uchanganuzi Usemi Hakiki (UUH) iliyoasisiwa na Fairclough katika kuchanganua hotuba sita za viongozi wawili wa kisiasa wa nchi ya Kenya kuhusu ufisadi ili kuchanganua na kulinganisha namna matini ya hotuba za kisiasa yanavyoshughulikia suala la ufisadi, kubainisha athari za hotuba hizi kwa wananchi na kisha kubaini mielekeo ya wananchi kuhusu hotuba hizi. Usampulishaji wa kimakusudi ulitumiwa kuwachagua wasailiwa na pia viongozi wa kisiasa ambao matini za hotuba zao zilichanganuliwa na kulinganishwa. Wanasiasa teule ni wale ambao wameliangazia suala hili la ufisadi kwa kina, hivyo basi hotuba zao ni faafu katika utafiti huu. Ili kupata matini za hotuba za kisiasa ambazo zilitumiwa kama data katika utafiti huu, mtafiti alikusanya video kutoka mtandao wa “YouTube”. Data nyingine pia ilikusanywa nyanjani kupitia hojaji funge ya likati na hojaji wazi ili kubaini athari na mielekeo ya wananchi wa Kenya kuhusu hotuba za kisiasa zinazoangazia suala la ufisadi. Mtafiti alizisikiliza na kuzinukuu hotuba teule kisha kuchanganua na kulinganisha matini zake. Aidha, data ilichanganuliwa na kulinganishwa kwa kutumia majedwali, takwimu na maelezo na kisha matokeo yake kuwasilishwa vilevile kwa kutumia maelezo, majedwali na takwimu. Matokeo ya utafiti huu yatawapa wananchi ama matumaini kuwa hotuba za kisiasa zinatekeleza dhima kuu katika vita dhidi ya ufisadi au ni gumzo tupu. Utafiti huu pia utachangia katika taaluma ya uchanganuzi matini ya hotuba za kisiasa zinazolenga maudhui teule kwa kutumia nadharia ya Uchanganuzi Usemi Hakiki.Item Kanuni za Lugha Zinavyoathiri Somo la Kiswahili Katika Shule za Upili: Mfano za Kaunti ya Busia(Kenyatta University, 2025-04) Osodo, Elizabeth Auma; King'ei, Kitula Osore, MiriamUtafiti huu ulishughulikia mielekeo ya wanafunzi na walimu wa shule za upili katika Kaunti ya Busia kuhusu kanuni za lugha shuleni na namna kanuni hizi zinavyoathiri somo la Kiswahili. Utafiti huu ulichunguza na kuhakiki kanuni za lugha katika shule za upili. Aidha ulibaini mielekeo ya wanafunzi na walimu kuhusu kanuni za lugha shuleni na athari yake kwa somo la Kiswahili. Malengo matatu yalioongoza utafiti huu ni: Kueleza kanuni za lugha shuleni, kuchunguza mielekeo ya wanafunzi na walimu kuhusu kanuni za lugha shuleni na kufafanua athari za kanuni za lugha shuleni kwa somo la Kiswahili katika shule zilizo Kaunti ya Busia.Utafiti huu ulitumia nadharia mbili katika uchanganuzi wa data. Kwanza, nadharia ya Saikolojia ya jamii ya Vitendo Vilivyofikiriwa ya Ajzen na Fishbein (1980). Nadharia hii inasema kuwa, binadamu huwa na mtazamo kubalifu kuhusu jambo ambalo litamnufaisha na kuwa na mwelekeo hasi kwa jambo ambalo halina manufaa kwake. Nadharia hii ilitumika kubainisha mielekeo ya walimu na wanafunzi kuhusu kanuni za lugha za shule. Nadharia hii haingeweza kuhakiki kanuni za lugha za shule na athari yake kwa somo la Kiswahili kwa kukosa vigezo vya kuchanganua data hii. Kwa hivyo, nadharia ya pili ambayo ni ya Kijumuia na Kibinadamu ilioasisiwa na Richards na Rodgers (1995) ilitumika. Nadharia hii inasema kuwa, mazingira yenye usalama na utu kwa mwanafunzi humwathiri anapojifunza lugha ya pili. Ili kufanikisha malengo ya utafiti, wanafunzi na walimu kutoka shule za upili saba zenye viwango vya Kitaifa, Zaidi ya Kaunti na Kaunti ziliteuliwa. Walimu na wanafunzi walijaza hojaji likati na wanafunzi kushiriki katika mjadala elekezi wa makundi. Utafiti huu ulihusisha wanafunzi 560 na walimu saba wa somo la Kiswahili ambao pia ni wakuu wa idara ya Kiswahili. Mtafiti pia alifanya mahojiano na walimu wakuu kwa kila shule kuhusu kanuni za lugha zilizoteuliwa. Utafiti uliteua shule tatu za wasichana za bweni, tatu za wavulana za bweni na shule moja ya mseto ya kutwa. Utafiti huu ulifanywa nyanjani na maktabani. Vifaa tofauti vilitumiwa nyanjani, hojaji likati ilitumika ili kubainisha mielekeo ya walimu na wanafunzi kuhusu kanuni za lugha za shule. Mjadala elekezi wa makundi ulitumika kubainisha sababu ya mielekeo chanya au hasi na manufaa ya kanuni za lugha za shule kwa wanafunzi. Mbinu ya uchunzaji ilitumika kwa kutazama mabango yaliyo shuleni na kuchunguza namna mijadala kwa lugha ya Kiswahili ilivyoendeshwa. Utafiti wa maktabani ulifanywa kwa kusoma kazi za waandishi mbalimbali zinazohusu sera ya lugha kwa jumla, kanuni za lugha shuleni pamoja na mielekeo yao. Uchanganuzi wa data ulifanywa kwa kuainisha mada tofauti tofauti. Njia ya maelezo ilitumika kuwasilisha data kwa kiasi kikubwa. Picha, majedwali na michoro pia ilitumika. Matokeo ya utafiti yalionyesha kuwa, shule tofauti zina kanuni za lugha tofauti na utekelezaji wake pia ni tofauti. Kanuni hizi ni kama lugha ya mawasiliano katika mazingira ya shule, siku za Kiswahili, mabango na maandishi katika mazingira ya shule, matumizi ya lugha ya Kiswahili katika mijadala, shughuli za idara ya Kiswahili kama makongamano, usomaji wa vitabu na magazeti pamoja na vyama vya Kiswahili. Ilibainika kuwa, wanafunzi na walimu wana mielekeo chanya kwa kanuni za lugha za shule ambazo zinaimarisha matokeo ya mtihani katika somo la Kiswahili. Utafiti pia ulibaini kuwa, utekelezaji wa kanuni za lugha za shule unahitaji mchango na ushirikiano wa wizara ya elimu, uongozi wa shule, walimu na wanafunzi wote ili athari yake iwe chanya kwa somo la Kiswahili.Item Itikadi Kama Chanzo cha Migogoro katika Msimu Wa Vipepeo K.W Wamitila (2006) na Mhanga Nafsi Yangu S.A Mohamed (2013).(Kenyatta University, 2025-04) Moses, Grace Mwende; King'ei, Kitula Osore, MiriamUtafiti huu ulishughulikia itikadi kama chanzo cha migogoro katika riwaya ya Msimu wa Vipepeo (2006) yake K.W Wamitila na Mhanga Nafsi Yangu (2013) yake S.A Mohamed. Utafiti huu ulinuia kuonyesha itikadi kama chanzo cha migogoro miongoni mwa wahusika katika riwaya teule. Tafiti tofauti zimefanywa na wataalamu kuhusiana na suala la migogoro katika riwaya ya Kiswahili. Hata hivyo, kadri ya ufahamu wa mtafiti haupo utafiti ambao umeangazia itikadi kama chanzo cha migogoro. Aidha, riwaya teule hazijachambuliwa kwa kuangazia mtazamo huu. Utafiti huu ulinuia kuchanganua itikadi kama chanzo cha migogoro katika riwaya teule, kutathmini athari za migogoro hii katika uwasilishaji wa maudhui na ploti katika riwaya na kujadili suluhu za migogoro hiyo kwa kuangazia riwaya teule. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Hejemonia iliyoasisiwa na mwanafalsafa Antonio Gramsci (1985). Mihimili ya nadharia hii ilikuwa ni, Hejemonia hutegemea makubaliano yaliyopo kati ya watawala na wanaotawaliwa, asasi za kijamii hutumiwa na tabaka tawala kuwapumbaza raia na Hejemonia huendelezwa kupitia kwa tamaduni za jamii husika. Mihimili hii ilimwezesha mtafiti kuichanganua data kwa ukamilifu. Mbinu ya kimaelezo ndiyo iliyotumiwa katika uchanganuzi wa data. Matokeo ya utafiti huu yameafikiana na yaliyotarajiwa katika utafiti huu kwa kudhibitisha kuwa itikadi ndizo chanzo cha baadhi ya migogoro iliyopo katika riwaya teule. Ni wazi kuwa, migogoro ambayo chanzo chake ni itikadi huibua maudhui tofauti na humsaidia mwandishi kuijenga ploti katika kazi yake. Mwisho, baadhi ya migogoro katika riwaya inaweza kusuluhishwa kwa kutumia mbinu tofauti ambazo ziliangaziwa. Matokeo ya utafiti huu yatakuwa ya manufaa kwa wasomi, watafiti na waandishi wa riwaya ya kiswahili kwa kukuza maarifa yao kuhusu suala la migogoro na itikadi za wahusika katika riwaya.Item Maudhui katika Nyimbo Zilizopendwa za Kiswahili: Mtazamo Linganishi wa Daudi Kabaka Na Kikundi cha Maroon Commandos(Kenyatta University, 2025-02) Malelu, Onesmus KiokoThe research intended to investigate themes in popular Swahili songs: A comperative approach of Daudi Kabaka and Maroon Commndos group. The songs were sang between the year 1960 and 1990. The research was guided by realism theory. The researcher went through recorded songs stored in round discs. Selected literary materials were also read for the purposes of getting data. The collected data was recorded and analysed guided by the research questions and objectives. The report was presented in five chapters. Chapter one includes the study topic, research questions, objectives of the study, justifications for the study, scope of the study, literature review and theoretical framework. The second chapter analyses themes in Daudi Kabaka and Maroon Commandos group songs. Chapter three examines how language use has aided in making the themes come out clearly. The fourth chapter examines the comparisons found between the works of the two artists. The fifth chapter includes summery, conclusion and recommendations for further research. This research will benefit other literary scholars and current artists to make their work better.Item Upokezi wa Taswira za Matangazo ya Biashara katika Runinga: Kata Ndogo za Nyali na Likoni Kaunti ya Mombasa, Kenya(Kenyatta University, 2025-06) Omuhonja, Elizabeth Nipher; King'ei, Kitula Osore, MiriamUtafiti huu ulichunguza upokezi wa taswira za matangazo ya biashara katika runinga. Matangazo kumi ya biashara yanayotangazwa kwa lugha ya Kiswahili yalichunguzwa pamoja na yale ambayo yanachanganya Kiswahili na lugha nyingine. Malengo ya utafiti huu yalikuwa ni kubainisha taswira zinazotumika kwenye matangazo yanayohusu bidhaa za nyumbani katika runinga, kuchanganua taswira zinazotumika kwenye matangazo yanayohusu huduma za mawasiliano katika runinga na kutathmini fasiri za watazamaji kuhusu taswira mbalimbali zilizoteuliwa kwa kuzingatia umri, jinsia na elimu. Sababu ya kufanya utafiti huu ni kuwa swala la kuonyesha namna mbinu ya taswira inavyotumika katika matangazo ya biashara kwa madhumuni ya kuathiri upokezi wa bidhaa zinazotangazwa halijachunguzwa kwa kina. Kazi hii iliongozwa na nadharia mbili; nadharia ya semiotiki iliyoasisiwa na Barthes (1984) inayohusu uhakiki wa ishara na nadharia ya ya upokezi iliyoasisiwa na Iser (1974) inayosisitiza nguvu za mpokeaji au msomaji katika kufasiri kazi anayoipokea na hutilia maanani dhima yake kwa kazi hiyo. Uchunguzi ulifanyika maktabani na nyanjani. Maktabani usomaji wa vitabu, tasnifu, makala na majarida yanayohusu mada ulifanyika kwa kina. Nyanjani data kuhusu fasiri mbalimbali za taswira ilikusanywa kwa kutumia hojaji katika maeneo ya Nyali na Likoni ili kuzitathmini. Matokeo ya utafiti yametolewa kwa njia ya kimaelezo na majedwali. Matokeo ya utafiti yalionyesha kuwa watangazaji wa matangazo ya biashara hutumia taswira kwa wingi katika matangazo hayo ili kupitisha ujumbe kwa hadhira. Taswira zinazotumika haswa za ishara huhitaji umakinifu wa hali ya juu kutoka kwa hadhira ili waweze kuzifasiri vyema. Taswira za ishara zilipata fasiri mbalimbali kutoka kwa hadhira kwa kuzingatia vigezo vya, umri, jinsia na kiwango cha elimu. Matokeo ya utafiti huu yamewasilishwa katika sura tano. Utafiti huu umetoa mchango kwa wasomi na watafiti kwa kuonyesha namna mbinu ya taswira inavyotumika katika matangazo ya biashara kwa lengo la kuathiri upokezi wake.Item Uchanganuzi wa Kiisimu katika Mashairi Huru ya Kithaka wa Mberia na ya Kezilahabia(Kenyatta University, 2025-06) Wafula, Pouline Nangila; King'ei, Kitula Osore, MiriamLengo kuu la utafiti huu ni kuonyesha jinsi ushairi unavyoweza kuchanganuliwa kiisimu. Tasnifu hii inahusu uhakiki wa kiisimu wa ushairi wa Kiswahili katika mashairi huru ya Kithaka wa Mberia na ya Kezilahabi kwa mtazamo wa nadharia ya Fonolojia Mizani. Utafiti huu umejikita katika diwani teule za watunzi waliotajwa ambazo ni Doa, Msimu wa Tisa, Mvumo wa Helikopta, Kichomi na Karibu Ndani. Uteuzi wa diwani hizi ulifanywa kimakusudi kwa kuwa zina aina data iliyodhamiriwa kuchanganuliwa kiisimu ambayo ilitosheleza mahitaji ya utafiti huu. Mashairi sitini yalihakikiwa kutoka katika diwani teule. Vipengele vya kiisimu vilivyochanganuliwa ni: Aina za sentensi, kipengele cha nafsi na uakifishaji. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Fonolojia Mizani iliyoasisiwa na Liberman (1975) ambayo ina madai kuwa mkazo katika lugha uko katika mfumo wa mfuatano wiani wa kimsonge ambao hupanga silabi, maneno na virai katika sentensi. Tasnifu hii ina sura nne: Sura ya kwanza imeangazia utangulizi unaojumulisha vipengele vifuatavyo: mada, suala la utafiti, maswala ya utafiti, malengo ya utafiti, umuhimu wa utafiti, sababu za kuchagua mada, upeo na mipaka ya utafiti, yaliyoandikwa kuhusu mada, misingi ya nadharia, mihimili ya nadharia na mbinu za utafiti. Sura ya pili imeshughulikia vipengele vya kiismu vilivyobainishwa na jinsi vinavyotumika katika kuendeleza kazi ya mashairi huru teule ya Kithaka wa Mberia. Sura ya tatu imebainisha vipengele vya kiisimu na kuonyesha jinsi vilivyotumika katika kuendeleza mashairi huru ya Kezilahabi. Sura ya nne imeshughulikia umuhimu wa vipengele vya kiisimu kisha sura ya tano imeshughulikia muhtasari wa utafiti, matokeo ya utafiti, changamoto za utafiti na mapendekezo ya taifi zaidi. Data iliyotumika katika utafiti huu ilikusanywa kutoka maktabani. Maktabani ndiko usomaji ulifanywaa wa diwani za mashairi teule, tasnifu na vitabu vingine vinavyohusiana na mada ya utafiti na nadharia ya utafiti huu. Uchanganuzi wa data ulifanywa kwa kutumia mbinu ya uhakiki matini kwa kuongozwa na pengo la utafiti, maswali na malengo ya utafiti na kwa kuongozwa na mihimili ya nadharia ya Fonolojia Mizani. Kwa kufanya hivi, utafiti uligundua kwamba mbinu za kiisimu zinaweza kutumiwa katika uhakiki wa mashairi huru ya Kiswahili.Item Usawiri wa Mandhari Katika Diwani ya Doa(Kenyatta University, 2025-06) Gitonga, Doris Gakii; King'ei, Kitula Osore, MiriamUtafiti huu ulishughulikia usawiri wa mandhari katika katika Diwani ya Doa na jinsi mandhari hayo yamechangia katika uwasilishaji wa ujumbe wa mwandishi. Utafiti huu ulilenga kubainisha jinsi mtunzi alivyotumia aina tofauti za mandhari katika kukamilisha ujumbe wake. Utafiti huu umebainisha wazi mandhari mbalimbali katika diwani ya Doa (2018). Aidha, utafiti hu umedhihihirisha namna mandhari hayo yalivyosawiriwa kwa kuweka wazi umuhimu wake katika kukamilisha ujumbe wa mtunzi. Utafiti huu ulichunguza aina za mandhari katika diwani ya Doa (2018). Nadharia ya Naratolojia ndiyo iliyoongoza utafiti huu. Naratolojia iliyoasisiwa na Genette (1972) na baadaye kuendelezwa na De Jong (2012). Nadharia ya Naratolojia huchunguza sifa za muundo wa usimulizi kwa kugawa vipengele ambavyo huhusiana na simulizi kisha kuzingatia uhusiano na uamilifu baina ya vipengele hivyo. Data iliyotumiwa katika uchunguzi huu ilitoka maktabani na mtandaoni. Kwa maktaba, mtafiti alisoma yale yanayohusiana na mada lengwa yakiwemo tasnifu, majarida na vitabu vinginevyo hasa vinavyo husiana na nadharia husika. Mtandaoni mtafiti alisoma baadhi ya tafiti zinazohusiana na mada teule na yanayohusu utanzu wa ushairi. Sampuli kusudio ni nakala ya diwani ya Doa (2018) ambayo ilikuwa muhimu sana katika utafiti huu. Yaliyotokea katika utafiti huu yametolewa kwa maelezo ya kinathari na utoaji wa mifano. Matokeo ya utafiti huu yamepangwa katika sura tano. Matokeo ya utafiti huu yanatarajiwa kuchangia pakubwa katika fasihi ya Kiswahili hasa utanzu wa ushairi kwa kuonyesha aina za mandhari na nafasi yake katika ukuzaji wa maudhui.Item Athari ya Tamthilia ya Mashetani (1971) juu ya Tamthilia ya Mashetani Wamerudi (2016)(Kenyatta University, 2025-05) Nyanchama, Filister EuniceUtafiti huu ulilenga kuchunguza athari ya tamthilia ya Mashetani (1971) juu ya tamthilia ya Mashetani Wamerudi (2016). Kristeva (1966) anafafanua kuwa hakuna matini yoyote ya kifasihi inaweza kuangaliwa kivyake au kujitegemea. Hivyo basi, ilikuwepo haja kuangazia athari ya dhamira, maudhui, wahusika na mtindo katika tamthilia hizi teule. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Mwingilianomatini ilioasisiwa na Kristeva (1966). Mwingilianomatini ni kutegemeana na kuathiriana kwa tanzu au matini (Kuloba, 2015). Hivyo basi, mwingilianomatini ni wakati ambapo sifa za matini moja huweza kujitokeza katika matini nyingine. Mtafiti aliongozwa na malengo yafuatayo: Kwanza, kubainisha athari ya kimaudhui katika tamthilia ya Mashetani na tamthilia ya Mashetani Wamerudi. Pili, kuchunguza athari ya usawiri wa kiwahusika katika tamthilia ya Mashetani na Mashetani Wamerudi. Tatu, kuchanganua athari ya kimtindo katika tamthilia ya Mashetani na tamthilia ya Mashetani Wamerudi. Mbinu ya utafiti iliyotumika ni ya kimaelezo ambapo mtafiti alibainisha matukio au data mbalimbali katika tamthilia ya Mashetani na Mashetani Wamerudi. Data iliyokusanywa iliwasilishwa kwa maelezo na kwa kutoa mifano ya maudhui, usawiri wa wahusika na mtindo kwenye tamthilia zilizoteuliwa. Mtafiti aliteua sampuli kimakusudi ili kufanikisha malengo ya utafiti. Utafiti ulikuwa wa maktabani ambapo mtafiti alisoma tamthilia husika, tasnifu, majarida na vitabu ambavyo vinahusiana na mada.Item Harakati Za Ushairi wa Kiswahili Katika Ujenzi wa Jamii Yenye Mabadiliko: Mfano wa Diwani Ya Karne Mpya(Kenyatta University, 2025-05) Gaceri, Martha; King'ei, Kitula Osore, MiriamUtafiti huu ulichunguza harakati za ushairi wa Kiswahili katika ujenzi wa jamii yenye mabadiliko. Mashairi yaliyorejelewa ni yaliyo katika Diwani ya Karne Mpya (2007). Malengo ya utafiti huu yalikuwa ni kubainisha miktadha iliyoibua harakati za ujenzi wa jamii yenye mabadiliko, kueleza harakati za ujenzi wa jamii yenye mabadiliko katika diwani teule, pamoja na kuonyesha umuhimu wa harakati hizo katika jamii. Utafiti huu uliongozwa na baadhi ya mihimili ya nadharia ya Uhistoria Mpya. Nadharia ya Uhistoria Mpya ina misingi yake katika mawazo ya Raymond Williams (1977) na Michel Foulcault (1972, 1977, 1997). Nadharia hii huangalia uhusiano uliopo kati ya historia na fasihi. Hivyo, kazi ya fasihi haiwezi kutengwa na historia inayohusika nayo. Utafiti huu ulichukua muundo wa kimaelezo. Utafiti ulifanywa maktabani na mitandaoni. Sampuli ya utafiti huu iliteuliwa kimakusudi na data ikakusanywa kwa kusoma kwa kina mashairi teule na kunukuu sehemu ambazo zina data iliyokidhi mahitaji ya utafiti husika. Mtafiti pia alisoma vitabu, majarida, tasnifu na machapisho mbalimbali yaliyohusiana na mada. Data ilichanganuliwa kwa kuzingatia malengo ya utafiti kwa kuongozwa na mihimili ya nadharia iliyoongoza utafiti huu. Matokeo ya utafiti huu yaliwasilishwa kwa njia ya maelezo ya kinathari na utoaji mifano. Utafiti huu ulibaini kuwa harakati mbalilmbali za ujenzi wa jamii yenye mabadiliko, zimeibuliwa na miktadha mbalimbali ya kiuchumi, kisiasa na kijamii. Isitoshe, harakati hizi zina mnachango muhimu katika jamii ya sasa. Inatarajiwa utafiti huu utachangia katika uhakiki wa fasihi kinadharia. Aidha, utaifaa jamii hasa katika kuelewa harakati za kujenga jamii yenye mabadiliko na manufaa yake. Tasnifu hii imegawika katika sura tano. Sura ya kwanza imeshughulikia utagulizi, usuli wa mada, suala la utafiti, malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, sababu za kuchagua mada, upeo na mipaka, yaliyoandikwa kuhusu mada nadharia iliyoongoza utafiti huu pamoja na mbinu za utafiti. Sura ya pili imeshughulikia miktadha iliyoibua harakati za ujenzi wa jamii yenye mabadiliko. Sura ya tatu imeshughulikia harakati za ujenzi wa jamii yenye mabadiliko. Sura ya nne imeshughulikia umuhimu wa ujenzi wa jamii yenye mabadiliko. Sura ya tano imeshughulikia hitimisho, matokeo ya utafiti, changamoto za utafiti pamoja na mapendekezo ya utafiti.Item Mtindo kwenye Nyimbo za Jadi Katika Jamii Ya Wakisii Na Waswahili wa Nchini Kenya(Kenyatta University, 2025-06) Oroko, Kerubo Judith; King'ei, Kitula Osore, MiriamMtindo ni uti wa mgongo katika tungo za kisanaa, iwe hadithi, tamthilia, ushairi na hata nyimbo. Utafiti huu umejikita katika kuhakiki mtindo kwenye nyimbo za jadi za jamii ya Wakisii na jamii ya Waswahili wa nchini Kenya. Watafiti mbalimbali wametafiti swala la mtindo katika nyimbo kama vile: Iyaya na wenzake (2021) walitafiti mtindo na lugha ya uwasilishaji katika nyimbo za nyiso za jamii ya Watachoni ambazo ni wenyeji wa Kenya. Muriuki (2013) alitafiti mtindo katika nyimbo za kazi katika jamii ya Warabai. Utafiti huu unatofautiana na tafiti za hapo awali hasa kwa msingi wa malengo na mambo mengine. Utafiti huu umefanikiwa katika: kubainisha jinsi ambavyo watunzi wametumia mbinu za mtindo katika kusawiri historian a tamaduni za jamii ya Wakisii na Waswahili wa nchini Kenya. Hali kadhalika, utafiti huu umehakiki mbinu za mtindo kwenye nyimbo za jadi za jamii ya Wakisii na Waswahili. Mwisho kabisa, utafiti huu umefanikiwa kuchunguza jinsi ambavyo mbinu za mtindo zilivyotumiwa kufanikisha uwasilishaji wa maudhui katika jamii teule. Nadharia ya mtindo ambayo iliasisiwa na Coombes ndiyo iliongoza utafiti huu. Coombes (1953) anasema kuwa mtindo huchunguza lugha na kanuni zinazoongoza lugha yenyewe ili kubainisha mbinu za kimtindo zilizotumiwa, sababu ya mbinu hizo kutumiwa na athari ya mbinu hizo katika kazi husika. Katika nadharia hii lazima mhakiki wa kazi yoyote ile ya fasihi achunguze vipengele hivyo na aelewe utendekazi wake. Waitifaki wengine ni kama Leech na Short (1981) ambapo wanasema kuwa nadharia hii ina lengo la kuelezea uhusiano uliopo baina ya lugha na majukumu ya kisanaa. Ambapo swali kuu ni mbona mwandishi akaamua kujieleza kwa njia fulani? Nyimbo za jadi za jamii ya Wakisii na Waswahili zilizotumiwa katika utafiti ziliteuliwa kwa kutumia mbinu ya maksudi ambapo nyimbo zenye ukwasi wa mtindo ndizo zilizingatiwa. Utafiti hulifanywa makatabni na nyanjani. Maktabani ulihusisha kusoma vitabu, tasnifu, matini na majaida kuhusu mtindo. Nyanjani ulijumuhisha kuwahoji watu kumi wakongwe kutoka kila jamii na kila jinsia ikiwakilishwa na watu watano watano. Hali kadhalika, hadhira ambayo ilishiriki katika uimbaji isailiwa ambapo watu wawili wawili kutoka kila sherehe walishirikishwa na mwisho kabisa watu wanne kutoka kila jamii ambao waliongozwa katika uimbaji wa nyimbo hizo walishirikishwa katika utafiti. Wawili wawili kutoka kwa kila jinsia. Mbali na hayo, mbinu ya kusikiliza na kurekodi nyimbo hio za jadi ilitumiwa baada ya hapo uchambuzi ukaanza. Data ilichanganuliwa kwa kuongozwa na mihimili ya nadharia, maswali na malengo ya utafiti. Kazi hii imepangwa katika sura tano. Utafiti huu uliweza kubainisha kuwa mbinu za mtindo zina nafasi kubwa katika kuendeleza nyimbo za jadi. Utafiti huu utakuwa na mchango mkubwa katika uwanaja wa fasihi simulizi kwa utawasadia wataalamu wa fasihi nawanafunzi wa fasihi kuchanganua na kuelewa mtindo katika nyimbo za jadi za jamii husika na pia katika kuhakiki mtindo katika tanzu zingine za fasihi simulizi.Item Matumizi ya Nyenzo za Kusikiliza na Kuona Katika Ufunzaji na Ujifunzaji wa Matamshi Katika Shule za Upill, Kaunti ya Kiambu, Kenya(Kenyatta University, 2022-10) Osore, Joy Lodenyi; King'ei, Kitula Osore, MiriamAbstractItem Uwasilishaji wa Maudhui ya Utamaduni Katika Riwaya Teule za Kiswahili(Kenyatta University, 2023-06) Kinyua Gatakaa Caroline; King'ei, Kitula Osore, MiriamAbstractItem Tathmini ya Viwango vya Maarifa ya Fasihi Katika Shule za Msingi, Kaunti ya Nyeri(Kenyatta University, 2022-04) Muriuki, Elizabeth Wangari; King'ei, Kitula Osore, MiriamAbstract