Uchambuzi wa matini: matumizi ya lugha ya kiswahili katika vivutio vya watalii
Loading...
Date
2016
Authors
Onyango, Everline Atieno
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Kenyatta University
Abstract
Utafiti huu umehusika na uchambuzi wa matini kwa kuangalia matumizi ya lugha katika
vivutio vya watalii. Utafiti huu ulichambua matini kwa kuzingatia muktadha wa
mawasiliano na hivyo ulijikita katika matini za kimazungurnzo. Katika vivutio vya
watalii, wahudumu na watalii walitumia lugha katika mawasiliano yao. Utafiti huu
umechanganua lugha katika mawasiliano baina ya wahudumu katika vivutio vya watalii
na watalii. Kwa hivyo, malengo ya utafiti huu yalijikita katika kuchanganua sifa bainifu
za lugha katika vivutio vya watalii, kubainisha athari za matumizi ya lugha katika vivutio
vya watalii kwa wasikizi na msimbo uliotumika katika vivutio vya watalii. Utafiti huu
uliongozwa na nadharia ya kidokezi maana fiche cha mazungurnzo iliyoasisiwa na Grice
(1975) ambayo inatazama matini kwa narnna ambavyo inakidhi mahitaji ya umilisi wa
mawasiliano na utoshelevu wa kipragmatiki. Nadharia ya kidokezi maana fiche cha
mazungurnzo ilitumiwa kulingana na malengo ya utafiti huu. Utafiti huu umekuwa wa
maktabani na nyanjani. Mtafiti alisoma maandiko kuhusu uchambuzi wa matini kisha
mtafiti alielekea nyanjani na alitumia mbinu ya uchunzaji ambapo alisikiliza mawasiliano
baina ya wahudumu katika vivutio vya watalii na watalii. Data za utafiti huu zilirekodiwa
kwa kutumia vinasa sauti. Utafiti ulionyesha kuwa vivutio vya watalii vina msimbo
wake, yaani wahudumu na watalii huzua narnna mbalimbali za kuwasiliana ili kupitisha
ujumbe kwa njia ya kipekee. Kuchanganya msimbo kulijitokeza mara tatu katika sentensi
kama mwazoni mwa sentensi, katikati ya sentensi na mwishoni mwa sentensi. Vile vile
kuchanganya msimbo kulitekeleza majukumufulani katika mawasiliano kama kusisitiza
jambo fulani, kurejelea na kufafanua. Ilibainika kuwa katika vivutio vya watalii huwa na
sifa za aina mbalimbali kama matumizi ya maswali, utohozi, ufafanuzi, takriri na
matumizi ya viziada lugha. Aidha, kulikuwa na athari ya matumizi ya lugha kwa wasikizi
katika vivutio vya watalii. Athari hizi zilikuwa mbili, nazo ni athari chanya na athari
hasi.Utafiti huu ulikuwa wa muhimu kwa sababu ulituonyesha sifa bainifu za lugha
katika vivutio vya watalii na hivyo basi kutambua jinsi wahudumu walivyoweza
kuwafanya watalii wengi kuzuru nchini kwa kutumia lugha.
Description
Tasnifu hii imetolewa ili kutosheleza baadhi ya mahitaji ya
shahada ya uzamili katika Chuo Kikuu cha Kenyatta