Matumizi ya jazanda katika tamthilia tatu za Timothy Arege

Loading...
Thumbnail Image
Date
2013
Authors
Okwena, Sophie
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Kenyatta University
Abstract
Utafiti huu umeshughulikia matumizi ya jazanda katika tamthilia za Chamchela ( 2007) , Mstahikiki Meya (2009) na Kijiba cha Mayo (2009) ambazo zimeandikwa na Timothy Arege. Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya kimtindo. Nadharia hii ilifaa utafiti huu hasa ikizingatiwa kwamba tamthilia hizi ambazo zimetafitiwa zimesheheni matumizi ya jazanda . Tasnifu hii ina sura sita. Sura ya kwanza imetupa mwelekeo wa utafiti wetu. Hapa tumejadili swala la utafiti, malengo ya utafiti na sababu za kuchagua mada. Hali kadhalika, sura hii imeshughulikia misingi ya nadharia, upeo na mipaka na yaliyoandikwa kuhusu mada. Mwisho ni mbinu za utafiti na uchanganuzi wa data. Sura ya pili inahusika na habari za mtunzi wa tamthilia tatu teule. Katika sura hii tumebainisha historia ya mwandishi ambapo wasifu wa mtunzi na masomo yake yamefafanuliwa. Aidha, mchango wake katika ulingo wa fasihi, waandishi wahornwathiri yote yamefafanuliwa dhahiri. Hatimaye, lugha yake, tajriba yake, utamaduni wake pamoja na muktadha wa lugha yake vimeshughulikiwa. Sura ya tatu imejadili maturnizi ya jazanda katika tamthilia ya Chamchela. Hapa turnejaribu kubainisha aina mbalimbali za jazanda ambazo mtunzi alitumia katika tamthilia hii. Aidha tumeonyesha namna mazingira ya mtunzi na lugha ya mtunzi yamechangia katika uteuzi wake wajazanda. Sura ya nne imechunguza matumizi ya jazanda katika tamthilia ya Mstahiki Meya. Hapa aina mbalimbali za jazanda ambazo mtunzi ametumia zimechunguzwa.Vivyo hivyo, mtunzi ameonyesha jinsi lugha na mazingira yake yalivyochangia katika maturnizi yake ya jazanda. Sura ya tano imejihusisha na matumizi ya jazanda katika tamthilia ya Kijiba cha Mayo. Utafiti umedhihirisha jinsi mwandishi ametumia jazanda za aina mbalimbali katika kuwasilisha ujumbe wake. Aidha, katika sura hii tumebainisha wazi namna lugha na mazingira ya mtunzi yalivyochangia pakubwa katika uteuzi wake wa jazanda. Sura ya sita ni muhtasari wa utafiti, mchango wa utafiti huu, changamoto za utafiti na hatimaye mapendekezo ya utafiti. Utafiti huu ni miongoni mwa tafiti chache ambazo zimewahi kuhakiki tamthilia za Chamchela, Mstahiki Meya na Kijiba cha Mayo kwa kutumia nadharia ya kimtindo. Utafiti huu utawasaidia wahadhiri na wanafunzi wa vyuo vikuu katika kuhakiki kazi zao. Hali kadhalika, utafiti huu utawasaidia walimu na wanafunzi wa shule za sekondari hususan kwa vile tamthilia ya Mstahiki Meya imeteuliwa kutahiniwa. Pia tunaamini kwamba utafiti huu utawasaidia wapenzi wote wa lugha ya Kiswahili.
Description
Tasnifu hii imetolewa u,i kutosheleza mahitaji ya shahada ya uzamili (M.A) katika Chuo Kikuu Cha Kenyatta 2013
Keywords
Citation