• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Uchanganuzi wa Kimofosintaksia wa Viangami Katika Lugha ya Kiswahili

Thumbnail
View/Open
Full text thesis (1.086Mb)
Date
2021
Author
Ndumba, Kimonye Naomi
Metadata
Show full item record
Abstract
Lengo la utafiti huu ni kushughulikia uchanganuzi wa kimofosintaksia wa viangami katika lugha ya Kiswahili. Utafiti huu ulilenga kuthihirisha kuwa kuna aina tofauti za viangami katika lugha ya Kiswahili. Viangami ni mofimu zinazojisimamia kisintaksia lakini kifonolojia ni tegemezi. Viangami hutegemea neno kuu kifonolojia. Viangami huambishwa kwa neno kuu. Kiangami ni sehemu ya neno kamili inayochukua nafasi ya kiambishi. Utafiti ulilenga kuchunguza changamoto katika uainishaji wa maneno yenye viangami, tofauti zilizopo katika uambishaji wa viambishi na viangami katika lugha ya Kiswahili, sheria za uundaji wa viangami na sifa arudhi za viangami. Nadharia iliyoongoza utafiti huu ni Nadharia Boreshaji ambayo iliasisiwa na Prince na Smolensky (1993). Kila sarufi inaweza kushughulikia maumboghafi tofauti. kwa mujibu wa nadharia hii, kunafaa kuwa na mfanano kati ya umboghafi na umbotokeo. Nadharia hii inajikita katika sifa bia za lugha zinazotumika kuunda miundo rasmi ya lugha. Ni kwa misingi hii ambapo utafiti huu ulijaribu kuchunguza kuwepo kwa viangami katika lugha ya Kiswahili. Utafiti huu ulifanyiwa maktabani. Katika maktaba, mtafiti alisoma kwa undani tafiti zilizofanywa na wanaisimu mbalimbali kuhusu viangami katika lugha tofauti. Vitabu vingine vilivyochapishwa na vimeshughulikia viangami vilipitiwa kwa undani. Vipengele vya utafiti vilivyohusishwa ni kama vile; mbinu za usampulishaji, sampuli iliyotumika iliteuliwa kimakusudi. Katika uteuzi wa sampuli, mtafiti aliteua vitabu tofauti. Mbinu za ukusanyaji wa data zilizotumiwa ni kusoma kwa kina makala kutoka maktabani. Mtafiti aliwasilisha matokeo yake kwa njia ya maelezo. Matokeo ya utafiti yaliwasilishwa kwa njia ya maelezo na majedwali. Kwa mujibu wa utafiti huu viangami vya Kiswahili vinaweza kuambishwa mwanzoni na mwishoni mwa neno. Viangami vinaambishwa kwa nomino, vitenzi, vihusishi na pia vielezi. Utafiti huu utaweza kurejelewa katika siku za usoni kuendeleza tafiti za ziada za viangami. Utafiti huu uliazimia kuwanufaisha wanaisimu kwani utaendeleza lugha ya Kiswahili. Wanafunzi wa lugha ya Kiswahili na waandishi wa vitabu vitabu vya Kiswahili pia watanufaika.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/22880
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback