• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Matumizi ya lugha katika sherehe za kumfunda mwali (dhifa za jikoni) miongoni mwa wazaramo

Thumbnail
View/Open
Full text thesis (74.04Mb)
Date
2011-11-02
Author
Mosha, Felician Doroth
Metadata
Show full item record
Abstract
Dhifa za jikoni ni sherehe zinazoadhimishwa katika makabila mengi nchini Tanzania. Sherehe hizi hutofautiana kwa kiasi fulani kulingana na kabila husika. Hii ni kwa sababu kila kabila lina utamaduni unaojibainisha na kabila jingine. Utafiti huu unahusu uchunguzi wa dhifa za jikoni katika jamii ya Wazaramo. Utafiti umehakiki matumizi ya tamathali za usemi. Tamathali mbili; tashibihi na sitiari ndizo zilizozingatiwa kwa kuwa zina nafasi kubwa katika sherehe hizo. Katika kufanikisha malengo ya utafiti, nadharia ya Ethnografia ya Mawasiliano imetumika katika uchanganuzi wa data. Data ilikusanywa kutoka mkoa wa Dar es Salaam katika mtaa wa Magomeni, nchini Tanzania. Mbinu ya kushiriki katika sherehe hizo ilitumika katika zoezi la kukusanya data, sanjari na matumizi ya hojaji na kanda zilizorekodiwa. Uchunguzi umedhihirisha kuwa matumizi ya tamathali hizo hubeba ujumbe mzito kwa mwali na kundi-jamii kwa jumla. Humsaidia mwali na hadhira kuupata vizuri ujumbe uliokusudiwa kwa njia fupi na kuufanya unate vizuri akilini na kuuhusisha na uhalisi wa kila siku wa maisha ya jamii. Pia husaidia hadhira kuendelea kuwa na motisha wa kusikiliza kinachowasilishwa. Vilevile imebainika kuwa wawasilishaji wa mawaidha wana mbinu bunifu za kuunda tashibihi na sitiari, huku wakizingatia vipengele vichache 'vya kitamaduni. Tamathali hizi zimeonekana kuwa na miundo ya wazi, kijazanda na kimethali. Swala la muktadha ndilo linalotawala mawasiliano katika Dhifa za jikoni na hivyo kuimarisha mawasiliano kati ya kundi-jamii hilo. Pia imegundulika kuwa baadhi ya vifaa vya upambaji na zawadi anazopewa mwali si katika matumizi ya kawaida tu, bali huashiria dhana fulani kimuktadha. Dhifa za jikoni ni uwanda ambao unahitaji tafiti zaidi za kitaaluma kutokana na majukumu yake kwa jamii. Inapendekezwa kuwa tafiti zifanywe katika vipengele vingine vya lugha na maudhui. Aidha, tafiti linganishi zifanywe kwa jamii zenye sherehe hizi. Kadhalika, Wazaramo wana sherehe za unyago na dhifa za jikoni. Hivyo, utafiti linganishi unahitajika katika sherehe hizi mbili.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/1529
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [241]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback