Repository logo
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Қазақ
  • বাংলা
  • हिंदी
  • Ελληνικά
  • Yкраї́нська
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
Repository logo
  • Communities & Collections
  • All of DSpace
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Қазақ
  • বাংলা
  • हिंदी
  • Ελληνικά
  • Yкраї́нська
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Wafula, Pouline Nangila"

Now showing 1 - 2 of 2
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Uchanganuzi wa Kiisimu katika Mashairi Huru ya Kithaka wa Mberia na ya Kezilahabia
    (Kenyatta University, 2025-06) Wafula, Pouline Nangila; King'ei, Kitula Osore, Miriam
    Lengo kuu la utafiti huu ni kuonyesha jinsi ushairi unavyoweza kuchanganuliwa kiisimu. Tasnifu hii inahusu uhakiki wa kiisimu wa ushairi wa Kiswahili katika mashairi huru ya Kithaka wa Mberia na ya Kezilahabi kwa mtazamo wa nadharia ya Fonolojia Mizani. Utafiti huu umejikita katika diwani teule za watunzi waliotajwa ambazo ni Doa, Msimu wa Tisa, Mvumo wa Helikopta, Kichomi na Karibu Ndani. Uteuzi wa diwani hizi ulifanywa kimakusudi kwa kuwa zina aina data iliyodhamiriwa kuchanganuliwa kiisimu ambayo ilitosheleza mahitaji ya utafiti huu. Mashairi sitini yalihakikiwa kutoka katika diwani teule. Vipengele vya kiisimu vilivyochanganuliwa ni: Aina za sentensi, kipengele cha nafsi na uakifishaji. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Fonolojia Mizani iliyoasisiwa na Liberman (1975) ambayo ina madai kuwa mkazo katika lugha uko katika mfumo wa mfuatano wiani wa kimsonge ambao hupanga silabi, maneno na virai katika sentensi. Tasnifu hii ina sura nne: Sura ya kwanza imeangazia utangulizi unaojumulisha vipengele vifuatavyo: mada, suala la utafiti, maswala ya utafiti, malengo ya utafiti, umuhimu wa utafiti, sababu za kuchagua mada, upeo na mipaka ya utafiti, yaliyoandikwa kuhusu mada, misingi ya nadharia, mihimili ya nadharia na mbinu za utafiti. Sura ya pili imeshughulikia vipengele vya kiismu vilivyobainishwa na jinsi vinavyotumika katika kuendeleza kazi ya mashairi huru teule ya Kithaka wa Mberia. Sura ya tatu imebainisha vipengele vya kiisimu na kuonyesha jinsi vilivyotumika katika kuendeleza mashairi huru ya Kezilahabi. Sura ya nne imeshughulikia umuhimu wa vipengele vya kiisimu kisha sura ya tano imeshughulikia muhtasari wa utafiti, matokeo ya utafiti, changamoto za utafiti na mapendekezo ya taifi zaidi. Data iliyotumika katika utafiti huu ilikusanywa kutoka maktabani. Maktabani ndiko usomaji ulifanywaa wa diwani za mashairi teule, tasnifu na vitabu vingine vinavyohusiana na mada ya utafiti na nadharia ya utafiti huu. Uchanganuzi wa data ulifanywa kwa kutumia mbinu ya uhakiki matini kwa kuongozwa na pengo la utafiti, maswali na malengo ya utafiti na kwa kuongozwa na mihimili ya nadharia ya Fonolojia Mizani. Kwa kufanya hivi, utafiti uligundua kwamba mbinu za kiisimu zinaweza kutumiwa katika uhakiki wa mashairi huru ya Kiswahili.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Umuhimu wa Vipengele vya Kiisimu katika Kuendeleza Kazi ya Mashairi Huru
    (East African Journal of Swahili Studies, 2025-04) Wafula, Pouline Nangila; Masinde, Edwin
    Makala hii imelenga kuchunguza umuhimu wa vipengele vya kiisimu katika kuendeleza kazi ya mashairi huru ya Kiswahili katika diwanı teule za Kithaka wa Mberia na Kezilahabi. Diwani teule zilizochanganuliwa ni: Doa, Mvumo wa Helikopta, Msimu wa Tisa, Kichomi na Karibu Ndani. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Fonolojia Mizani ambayo iliasisiwa na Liberman (1975) na kuendelezwa na Liberman na Prince (1977), Nadharia ya Fonolojia mizani inadai kuwa mkazo katika lugha uko katika mfumo wa mfuatano wiani wa kimsonge ambao hupanga silabi maneno na virai katika sentensi. Vipengele vya kiisimu vilivyochanganuliwa ni: aina za sentensi, kipengele cha nafsi na uakifishaji. Utafiti huu ulitumia sampuli ya kimakusudi katika kuteua diwani teule. zilizohakikiwa. Data Iliyotumika katika utafiti huu ilikusanywa kutoka maktabani. Ni Maktabani ndiko tuliweza kusoma mashairi kutoka katika diwani teule, nadharia ya utafiti na vitabu vingine vinavyohusiana na mada ya utafiti huu. Uchanganuzi wa data ulifanywa kwa kutumia mbinu ya uhakiki matini kwa kuongozwa na pengo la utafiti. Matokeo ya utafiti yaliwasilishwa kwa njia ya maelezo yaliyoambatanishwa na mifano ya beti mwafaka za mashairi kutoka katika diwani teule. Matokeo ya utafiti huu yameonyesha kuwa vipengele vya isimu vinachangia pakubwa katika kuendeleza kazi ya mashairi huru ya Kiswahili. Utafiti lengwa umechangia katika taaluma ya ushairi kwa kuelewa umuhimu wa vipengele vya kiisimu katika kuendeleza kazi ya mashairi huru ya Kiswahili. utafiti huu unapendekeza wasomaji wa mashairi, huru wazingatie matumizi ya vipengele vya kiisimu katika kuendeleza kazi ya mashairi huru ya Kiswahili.

DSpace software copyright © 2002-2025 LYRASIS

  • Cookie settings
  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback