Tathmini ya hadithi za watoto katika mtandao

Loading...
Thumbnail Image
Date
2015
Authors
Gatwiri, Joy Njue
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Kenyatta University
Abstract
Utafiti huu ulinuia kutathrnini hadithi za watoto katika mtandao. Hadithi mbalimbali za watoto zilichunguzwa arnbazo ni: visasili, hekaya, hurafa na hadithi zinazotokana na methali. Njia rnbalimbali za matumizi ya mtandao ziliangaziwa arnbazo ni matumizi ya mtandao kama kifaa cha kutolea matangazo na waandishi na wachapishaji ambao huonyesha bei mbalimbali ya vitabu. Pia mtandao kama maktaba ambapo watoto wanaweza kutumia muda wao kuzisoma hadithi katika mtandao. Pia nj ia tofauti ambazo zimetumiwa kuwasilisha hadithi hizo ambazo ni kwa maandishi ambayo yanaweza kusomwa na matumizi ya vielelezo. Utafiti pia uliangazia hadithi ambazo zimechapishwa na zile arnbazo hazijachapishwa. Nadharia ya utegernezi wa vyombo vya habari ya Ball- Rokeach na Defleaur (1976) ilitumika ambayo ilisaidia kuelewa jinsi hadithi za watoto zinavyoingiliana na vyombo vya habari ili kutirniza malengo matatu ambayo ni maelewano, burudani na ufunzaji. Nadharia ya fasihi ya watoto ya J ungmeen (1999) pia itatumiwa ili kuelewa jinsi fasihi ya watoto inavyotangamana na maendeleo ya teknolojia. Utafiti huu uliendelezwa katika maktaba na kutalii tovuti mbalimbali . Utafiti huu ulikuwa wa kimaelezo na ufafanuzi. Mbinu ya jumla ilitumika katika kuchanganua data.
Description
Tasnifu iliyowasilishwa katika idara ya kiswhili na lugha za Kiafrika katika Chuo Kikuu cha Kenyatta kwa minajili ya kutosheleza baadhi ya mahitaji ya shahada ya uzamili, 2015
Keywords
Citation