Matumizi ya Filamu Katika Kufunzia Sarufi ya Kiswahili Nchini Kenya

Loading...
Thumbnail Image
Date
2025-01
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
East African Journal of Swahili Studies,
Abstract
Makala haya yananuia kuchunguza uwezekano wa kutumikiza filamu ili kuimarisha utendaji wa sarufi katika lugha ya Kiswahili. Ni wajibu wa mwalimu kuteua matumizi ya nyenzo inayomwezesha kuibua mazingira halisi ya kufunzia sarufi darasani. Hata hivyo licha ya wanafunzi katika jimbo la Nyeri kutumia lugha ya Kiswahili katika shughuli zao za kila siku matokeo ya mtihani katika somo la Kiswahili hasa katika mtihani wa KCSE yalikuwa dhaifu mnamo katika mwaka wa 2019. Hii ndiyo sababu iliyomchochea mtafiti wa kazi hii kuchunguza matumizi ya filamu na athiri zake kwa utendaji wa wanafunzi katika lugha ya Kiswahili katika shule za upili. Wanafunzi katika shule za upili hawajakuwa wakifanya vyema katika karatasi ya Sarufi. Kulingana na wataalamu filamu imekuwa ikitumikizwa katika kufunzia lugha ya Kingereza huko Umarekani na Uingereza na pia somo la Hisabati katika Afrika Kusini ambapo iliripotiwa kwamba wanafunzi waliotumikiza filamu walifanya vyema katika kujifunza Kingereza na Hisabati. Nchini Kenya filamu imekuwa ikitumikizwa na walimu katika kufunzia somo la Fasihi na hivyo kubagua kipengele cha sarufi. Pengo hili liliibua haja ya kutafitia matumizi ya filamu katika kufunzia sarufi ya Kiswahili angalao kuboresha matokeo ya karatasi ya pili yaani inayojulikana kama sarufi au Matumizi ya Lugha. Makala haya yaliongozwa na Nadharia ya utabia ya Hermer (1996), kupitia kwa mihimili yake tofauti. Utafiti huu ulitekelezwa maktabani na nyanjani. Utafiti wa maktabani ulichangia kutambua usuli wa matumizi ya filamu ulimwenguni. Utafiti wa nyanjani ulifanyika katika eneo la Mukurweini linaloakilisha jumuiya ya wanafunzi wanaotumia silibasi sawia na wanafunzi wengine kote nchini Kenya. Sampuli zilizotumikizwa ziliteuliwa kimakusudi na kwa njia za kuelezea. Katika ukusanyaji data utafiti huu ulizingatia mbinu za hojaji, Uchunzaji na mtihani kwa wanafunzi. Data iliyokusanywa ilichanganuliwa na kuwasilishwa kupitia michoro na maelezo tofauti. Kufuatia jinsi wanafunzi wamekuwa wakipata gredi dhaifu katika sarufi kwa muda wa miaka mitano mfululizo. Kwa majubu wa matokeo ya utafiti....
Description
research article
Keywords
Citation
Mburu, R., Babusa, H. O. & Ngugi, B. (2025). Matumizi ya Filamu Katika Kufunzia Sarufi ya Kiswahili Nchini Kenya. East African Journal of Swahili Studies, 8(1), 90-104. https://doi.org/10.37284/jammk.8.1.2628