Uhuru wa kishairi katika utunzi wa mashairi: uchanganuzi wa sikate tamaa na miale ya uzalendo

Loading...
Thumbnail Image
Date
2016-05
Authors
Munyao, Meshack Kimeu
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Kenyatta University
Abstract
Utafiti huu ulishughulikia matumizi ya uhuru wa kishairi katika utunzi wa mashairi: uchanganuzi wa Miale ya Uzalendo na Sikate tamaa. Utafiti huu ulifanywa kwa lengo la kuwasaidia wasomaji wakiwemo walirnu na wanafunzi kuuelewa ushairi wa Kiswahili. Utafiti huu 'uliongozwa na malengo haya: kubainisha mbinu mbalimbali za uhuru wa kishairi, kuonyesha namna uhuru wa kishairi unavyobainika katika kazi hizi mbili na kueleza sababu za msanii kutumia uhuru wa kishairi. Ili kuyafikia malengo haya utafiti huu uliongozwa na nadharia ya upokezi. Nadharia hii inamwangazia msomaji na tajriba yake ya kazi ya fasihi tofauti na nadharia za zamani zilizolenga mwandishi na matini yen yewe. Nadharia hii inamtambua msomaji kama kiungo muhimu ambacho kinaipa kazi ya fasihi kuweko na hivyo kukaniilisha maana yake kupitiaufasiri rnwema-Utafiti huu ulifanyiwa maktabani. Pia huduma za rntandao zilitumiwa hasa kupata wasifu wa waandishi wa diwani hizi na maelezo zaidi ya nadharia. Vitabu vilivyochunguzwa ni Miale ya Uzalendo na Sikate Tamaa. Tasnifu hii ina sura tano. Sura ya kwanza ina sehemu zifuatazo; utangulizi wa tasnifu, mada ya utafiti, madhumuni ya utafiti, sababu za kuchagua mada, upeo na mipaka ya utafiti, udurusu wa mada, misingi ya nadharia na mbinu za utafiti. Sura ya 'pili imeshughulikia sifa za ushairi wa Kiswahili hasa lugha na ushairi wa Kiswahili. Aidha imeangazia wasifu wa wasanii; Mohamed S.A na Kitula King'ei. Mwishowe ikaangazia mbinu mbalimbali za uhuru wa kishairi zinazotumika katika utunzi wa mashairi. Katika sura ya tatu, tasnifu imeangazia matokeo ya utafiti; yaani jinsi uhuru wa kishairi ulivyo tumika katika diwani; Miale ya Uzalendo ya King'ei (1999). Sura ya nne imeonyesha namna uhuru wa kishairi ulivyotumika katika Sikate Tamaa ya Mohamed (1980). Sura ya tano imetoa muhtasari, hitimisho na mapendekezo ya utafiti. Utafiti huu ni miongoni mwa tafiti chache ambazo zimefanywa kuhusuuhuru wa kishairi. Utafiti utawafaidisha wasomi wengi wakiwemo wahadhiri, walimu 'na wanafunzi wanaotafuta uelewa wa ushairi wa Kiswahili. Aidha utawafaa wahakiki wengi wa fasihi ya Kiswahili hususan mashairi.
Description
Tasnifu hii lmetolewa kwa idara ya kiswahill na lugha za katika Chuo Kikuu cha Kenyatta kwa minajili ya kutosheleza baadhi ya mahitaji ya shahada ya uzamili katika kiswahili. May 2016, The PL 8704 .M82
Keywords
Citation