Mwananchi wa kawaida kama mdhulumu wa maslahi yake katika tamthilia za Kilio Cha Haki, Amezidi na Mstahiki Meya.
Loading...
Date
2018-03
Authors
Omoga, Ronic Gaddafi
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Kenyatta University
Abstract
Utafiti huu ulichanganua kazi za Al- Amin Mazrui, Timothy Arege na Said
Ahmed Mohamed ambazo ni tamthilia za Kilio cha Haki (1981), Mstahiki
Meya (2009) na Amezidi (1995) mtawalia. Kazi hizi zililenga kumsawiri
mwananchi wa kawaida kama chanzo cha dhuluma dhidi yake. Kwa kutumia
sifa mbalimbali za wahusika, kazi hizi zinaangazia maisha ya wananchi katika
nchi zinazoendelea hasa katika kipindi cha ukoloni na baada ya ukoloni. Utafiti
huu unapania kuonyesha kuwa shida wanazokumbana nazo wananchi katika
mataifa yanayoendelea zinatokana na wananchi wenyewe. Kwa hivyo, utafiti
umebainisha baadhi ya matendo wanayoshiriki wananchi ambayo yanawafanya
wajidhulumu. Nadharia ambazo ziliongoza utafiti huu ni nadharia ya uhalisia
wa kijamaa ya Friedrich Hegel na nadharia ya udenguzi ya Jacques Derrida .
Nadharia ya udenguzi imeasaidia katika kubainisha jinsi maoni ya waandishi
wengi kuhusu chanzo cha dhuluma kwa mwananchi si ya hakika. Waandishi
wengi wanahusisha kuteseka kwa mwananchi na umaskini, uongozi mbaya,
mila zilizopitwa na wakati miongoni mwa sababu nyingine. Utafiti unalenga
kuonyesha kuwa kwa kiwango kikubwa, ni mwananchi aliye chanzo cha
dhuluma anazokumbana nazo. Nadharia ya uhalisia wa kijamaa imemwezesha
mtafiti kuhakiki na kuchambua hali na maisha halisi ambamo wananchi wa
kawaida hujidhulumu. Utafiti huu ulifanywa maktabani na tamthilia teule
zilichaguliwa kwa njia makusudi ikilenga tamthilia za Mstahiki Meya, Kilio
cha Haki na Amezidi. Matokeo ya utafiti yamewasilishwa kwa maelezo kwa
kufuata utaratibu huu: sura ya kwanza ya utafiti imetanguliza mada, maswali
yanayoongoza utafiti, malengo ya utafiti, upeo na mipaka, yaliyoandikwa
kuhusu mada, sababu za kuchagua mada na misingi ya nadharia. Sura ya pili
ilihusu chanzo cha dhuluma kwa mwananchi wa kawaida. Sura ya tatu
ilishughulikia athari zinazotokana na dhuluma kwa mwananchi kwa kuangazia
tamthilia teule. Sura ya nne ilishughulikia mikakati ya mwananchi katika
kuzuia dhuluma nayo sura ya tano ilishughulikia matokeo ya utafiti pamoja na
mapendekezo ya mtafiti. Inatarajiwa kuwa utafiti huu umekuwa wa manufaa
katika kuonyesha nafasi aliyonayo mwananchi katika kujikomboa au
kujidhulumu. Aidha, utafiti huu utakuwa wa muhimu kwa wananchi kufahamu
nafasi zao katika kubainisha uongozi bora.
Description
Tasnifu hii imetolewa ili kutosheleza baadhi ya mahitaji ya Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Kenyatta. Machi, 2018