Taswira ya Malezi ya Watoto Katika Riwaya za Tumaini (2006) na Dunia Mashaka Makuu (2004)

dc.contributor.advisorKing'ei, Kitula Osore, Miriam
dc.contributor.authorMwenda, Agnes Kananu
dc.date.accessioned2021-02-25T07:42:12Z
dc.date.available2021-02-25T07:42:12Z
dc.date.issued2020-03
dc.descriptionTasnifu hii Imewasilishwa Katika Idara ya Kiswahili na Lugha za Kiafrika ya Chuo Kikuu cha Kenyatta ili Kutoshelesha Baadhi ya Mahitaji ya Shahada ya Uzamili. Machi, 2020en_US
dc.description.abstractUtafiti huu unalenga kuchunguza taswira ya malezi ya watoto katika riwaya mbili za Kiswahili ambazo ni: Tumaini ya Clara Momanyi (2006) na Dunia Mashaka Makuu ya Lamin Omar (2004) Malezi ya watoto ni mambo halisi yanayoikumba jamii ya kisasa ambayo inapitia mabadiliko mengi. Mabadiliko haya huwa ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, kidini na kiteknolojia. Waandishi wa riwaya huteua masuala yenye mguso kwa jamii na kuyasimulia kwa kiwango cha juu cha ubunifu. Utafiti huu uliongozwa na maswali yafuatayo: Ni mbinu zipi za malezi zinazobainika katika riwaya teule? Ni asasi na hali gani zinazochangia katika malezi ya watoto? Mbinu za malezi zina athari gani kwa watoto katika riwaya teule? Utafiti huu uliongozwa na malengo yafuatayo: Kueleza aina ya malezi yanayobainika katika riwaya teule, kubainisha asasi na hali za jamii zinazochangia katika malezi ya watoto katika riwaya teule na kueleza athari za mbinu za malezi zinazobainika katika riwaya teule. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya uhalisia ya Gustave Flaubert (1850). Baadhi ya waitifaki wa nadharia hii ni Rene wellek (1960), Hegel (1971) na Lukacs (1979). Nadharia ya uhalisia inaeleza kuwa kazi ya msanii inapaswa kuwasilisha ukweli kama ulivyo katika mazingira. Baadhi ya mihimili ya nadharia hii ni: Matukio yanayosimuliwa sharti yawe yanatokea katika ulimwengu halisi, kazi ya msanii inapaswa kuonyesha hali ya kisaikolojia ya wahusika ambao msomaji anakumbana nao na jinsi wanavyohisi na kutenda wanapokumbana na hali Fulani na wahusika huwa halisi na lugha wanayotumia huwa rahisi. Huku mtafiti akiongozwa na mihimili ya nadharia alihakiki riwaya zilizoteuliwa ili kupata data iliyotoshelesha mahitaji ya utafiti huu. Uteuzi wa sampuli ulitumika na riwaya mbili ziliteuliwa: Tumaini ya Clara Momanyi (2006) na Dunia Mashaka Makuu ya Lamin Omar (2004). Riwaya hizi zilitupa data faafu katika utafiti huu. Utafiti huu ulifanywa maktabani. Mtafiti alisoma kwa kina vitabu vya fasihi, majarida na tasnifu zilizoandikwa awali ili kufanikisha kazi yake. Data iliyopatikana ilichanganuliwa kulingana na malengo na maswali ya utafiti pamoja na mihimili ya nadharia. Data iliwasilishwa kwa maelezo katika sura tano. Utafiti huu umekusudiwa kuwafaa wanafunzi, walimu, wahakiki na waandishi wengine katika kubainisha umuhimu wa kuwapa watoto malezi mema. Pia, utawafaidi walezi na jamii kwa jumla.en_US
dc.identifier.urihttp://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/21623
dc.language.isoKiswahilien_US
dc.publisherKenyatta Universityen_US
dc.subjectTaswiraen_US
dc.subjectMalezi ya Watotoen_US
dc.subjectRiwaya za Tumaini (2006)en_US
dc.subjectDunia Mashaka Makuu (2004)en_US
dc.titleTaswira ya Malezi ya Watoto Katika Riwaya za Tumaini (2006) na Dunia Mashaka Makuu (2004)en_US
dc.typeThesisen_US
Files
Original bundle
Now showing 1 - 1 of 1
Loading...
Thumbnail Image
Name:
Taswira ya malezi ya watoto....pdf
Size:
521.87 KB
Format:
Adobe Portable Document Format
Description:
Full text Thesis
License bundle
Now showing 1 - 1 of 1
No Thumbnail Available
Name:
license.txt
Size:
1.71 KB
Format:
Item-specific license agreed upon to submission
Description: