Utomilisi wa Lugha Kama Chanzo cha Ubadilishanaji Msimbo Miongoni mwa Wanafunzi wa Chuo Kikuu Katika Kaunti ya Kiambu

Loading...
Thumbnail Image
Date
2022
Authors
Mwai, Beatrice Njambi
Chacha, Leonard
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
East African Nature and Science Organization
Abstract
Utafiti huu ulichunguza swala la kubadili msimbo miongoni mwa wanafunzi wa vyuo vikuu Kaunti ya Kiambu. Fikra kuu iliyoongoza utafiti huu ni kuwa wanafunzi hao hubadili msimbo kwa sababu ya utomilisi wa lugha. Hawana umilisi mkamilifu wa lugha moja. Kwa mfano, utafiti huu umeangazia lugha za Kiingereza na Kiswahili. Tumedhihirisha kuwa hawa ni wanafunzi wa chuo kikuu lakini hawawezi kuwasiliana kwa lugha moja kwa ufasaha, lazima waingie katika lugha nyingine ili kufanikisha mawasiliano. Kwa mfano, kama wanatumia lugha ya Kiswahili wanabadilisha na kuingia katika lugha ya Kiingereza kwa sababu wameshindwa kuendeleza mazungumzo katika lugha ya Kiswahili. Utafiti huu umeongozwa na nadharia tambulishi iliyopendekezwa na Myers-Scotton (1983). Kulingana na Myers-Scotton, katika mawasiliano yoyote, kuna hali ya alama inayotambulika na isiyotambulika. Katika kuchagua alama, mzungumzaji huchagua alama kulingana na mahitaji ya kijamii. Pia huonyesha kuwa kubadili msimbo ni kwa sababu ya ugumu wa watu kutumia lugha moja na ugumu huo uko akilini mwa mzungumzaji. Utafiti huu umeegemea maktabani na nyanjani. Maktabani, utafiti huu umenufaika kwa kupata data kutoka kwa machapisho, vitabu na majarida kuhusu dhana ya kubadili msimbo, uwili lugha na misingi ya nadharia. Nyanjani, utafiti huu umefanywa katika Kaunti ya Kiambu, Chuo Kikuu cha Kenyatta na Chuo Kikuu cha Mount Kenya. Utafiti huu umehusisha matumizi ya vifaa kama vile mwongozo wa mahojiano na kuhudhuria vikao rasmi ambavyo vijana wanawasiliana. Data iliyochanganuliwa kwa mujibu wa nadharia tambulishi imewasilishwa kwa njia ya maelezo
Description
Article
Keywords
Kubadili msimbo, Umilisi wa Lugha, Utomilisi wa Lugha, Wingi Lugha
Citation
Mwai, B. N., & Chacha, L. (2022). Utomilisi wa Lugha kama Chanzo cha Ubadilishanaji Msimbo Miongoni mwa Wanafunzi wa Chuo Kikuu katika Kaunti ya Kiambu. Jarida la Afrika Mashariki la Masomo ya Kiswahili, 5(1), 64-72.