• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Mashairi huru: uchambuzi wa dhamira na mtindo

Thumbnail
View/Open
Full Text Thesis (65.15Mb)
Date
2012-05-08
Author
Masinde, Edwin
Metadata
Show full item record
Abstract
Tasnifu hii inashughulikia baadhi ya mashairi huru ya watunzi atatu wa tanzania. Inajadili dhamira na mtindo katika mashiri huru ya kiswahili, hususa jinsi dhamira zinavyoathiri uteuzi wa ligha katika kazi ya fasihi na hasa ushairi. Tumejaribu kuonyesha kwamba dhamira ya mtunzi na mtindo anaotumia katika kutoa ujumbe wake ni vipengele vinavyotegemeana. Mtunzi atunga kutokana na tajriba aliyopata katika mazingira yake na lugha ndiyo njia aitumiayo kuyaeleza mambo mbalimbali ya jamii yake kea njia ya kubuni. Mazingira ya mwandishi katika ujumla wake huathiri uteuzi wake wa ligha na mitindo anayoitumia . Katika tasnifu hii, tumejaribu kuonyesha uwiano huu na kudhihirisha kwamba ijapokuwa ushairi huru unatofautianal katika muundo wa nje na ushairi wa jadi, sifa za aina hizi mbili za ushairi ni sawa hasa tukiazingatia umbo la ndani. Aidha tumejaribu kunyesha kuwa mtindo wa mwandishi huathiri uibushaji wa ujumbe wake. Sura ya kwanza ni utangulizi ambao ni muhtasari wa mwongozo uliotusaidia katika utafiti na uchambuzi wa mashairi-huru tuliyochagua. Kati ya mambo ambayo yamejadiliwa katika sehemu hii ni somo la utafiti, madhumuni ya utafiti na msingi wa nadharia. Pia tumeeleza upeo wa tasnifu na kujadili kazi mbalimbali ambazo zimeshughulikia somo hili. Sura ya pili inajadili mazingira walimotungia washairi tuliowachagua. Tunaafiki maoni ya Senkoro (1987: 1) kwamba misingi na mikondo ya historia ya jamii huipa fasihi umbo kimaudhui na kifani pamoja na mwelekeo. Rene Wellek na Austin Warren (1949: 94-95) wanasisitiza kauli hii kwa kusema: - Fasihi ni asasi ya kijamii inayotumia lugha; ni ubunifu wa Kijamii. Vipengele vya fasihi kama taswira na mdundo vinatokana na jamii. Wahakiki hawa wanachosisitiza ni kwamba fasihi haiibuki katika ombwe tupu. Hivyo, mhakiki wa fasihi hana budi kuzingatia mazingira ya kijamii ili kugundua vipengele vinavyoihuisha kazi fulani. Ni katika muktadha huu ambapo tunasisitiza kwamba mazingira ya kihistoria ya Tanzania, yawe ya kijamii, kiuchumi au kisiasa, yameathiri kazi za washairi hawa kidhamira na kimtindo. Ushairi kama kazi ya sanaa utaeleweka na kutathminiwa vyema zaidi katika mazingira ya wakati maalum wa kihistoria. Pia fasihi hupata uhai wake kutokana na hali halisi za jamii. Hivyo basi katika sura hii, tumejadili mazingira ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya Watanzania katika vipindi viwili muhimu; wakati wa ukoloni na baada ya ukoloni. Tumejadili kipindi cha uhuru katika viwango viwili: Kabla na baada ya Azimio la Arusha la mwaka 1967. Lengo letu hapa ni kuonyesha jinsi matukio muhimu katika vipindi hivi yalivyoathiri mifumo ya kijamii ya Watanzania na kuathiri fasihi yao katika vipengele vyote. Katika sura ya tatu, tumechambua mashairi yenye maudhui ya kisiasa. Tumeonyesha jinsi maudhui ya mtunzi yalivyosababisha uteuzi maalum wa lugha katika kuyaibusha. Sura ya nne imejadili uchambuzi wa mashairi yenye maudhui ya uchumi. Katika sehemu hii, tumeonyesha jinsi uteuzi wa mtindo maalum wa mwandishi unavyosaidia kuibusha dhamira na jinsi dhamira pia inavyoathiri uteuzi huu. Katika sura ya tano, tumechambua mashairi yenye maudhui ya maswala mengine ya kijamii kama vile ndoa, mapenzi, dini, utamaduni na falsafa kuhusu maisha. Tumeonyesha namna maudhui hayo yalivyojengwa kifani. Imedhihirika kwamba umbo la ndani la shairi ni muhimu katika kueleza maana yake. Sura ya sita ni hitimisho. Sura hii ni muhtasari wa matokeo ya utafiti wetu ambamo licha ya kueleza ugunduzi wa uchambuzi wetu, tumetoa kauli yetu juu ya ushairi-huru na mashairi-huru, na maeneo ambayo yanastahili kufanyiwa utafiti zaidi hapo baadaye.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/4519
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback