• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Matatizo ya kisarufi miongoni mwa wanafunzi wa Kikipsigis wanaojifunza Kiswahili sanifu: mtazamo wa lugha kadirifu

Thumbnail
View/Open
Full Text Thesis (56.06Mb)
Date
2012-03-29
Author
Chepkwony, Leonard Cheruiyot
Metadata
Show full item record
Abstract
Lengo kuu la kazi hii ni kuchunguza matatizo ya kisarufi miongoni mwa wanafunzi wa Kikipsigis wanaojifunza .Kiswahili Sanifu. utafiti huu ulifanywa kwa kutumia. misingi ya nadharia za Lugha Kadirifu na Uchanganuzi Makosa. Nadharia ya Lugha Kadirifu hurejelea maumbo ya muda mfupi ya kisarufi yanayoundwa na wanafunzi wa lugha ya pili wanapojaribu kujifimza lugba hiyo. Nadharia hii huchukulia kuwa, lugba ya mwanafunzi hupitia viwango kadhaa kabla ya kufikia kwenye ukamilifu wa ujuzi wa lugha ya pili. K wa kutumia misingi ya nadharia bizi, tumebaini ehanzo, aina na kiasi eha kutokea kwa makosa ya wanafunzi wa Kikipsigis wanaojifunza Kiswahili Sanifu na kupendekeza mikakati ya ufundishaji inayoweza kutumiwa iIi kupunguza au kuondoa makosa hayo. Katika utafiti huu, mbinu zifuatazo zilitumiwa kukusanyia data: Hojaji, mahojiano na utazamaji. Majaribio manne yalitumiwa. Jaribio la kwanza lilihusu kutafsiri sentensi za Kikipsigis kwa Kiswahili. Jaribio hili lilijaribu kuehunguza iwapo kuna athari za Kikipsigis katika matumizi ya Kiswahili. Jaribio la pili lilikuwa ni kujaza mapengo yaliyoachwa wazi katika sentensi. Jaribio hili lilifaa iii kudlubiti wanafunzi kwa kuwalazimisha watoe majibu kulingana na matakwa ya mtafiti. Jaribio la tatu lilihusu uandishi wa insha. Wanafunzi walihitajika kuandika insha ya ukurasa mmoja juu ya 'Kijiji ehetu.' Jaribio la mwisho lilihusu kusikiliza na kumngumza. Mwanafunzi alihitajika kusimulia kwa kifupi hadithi anayoipenda huku mtafiti akinasa kwa kanda. Utafiti huu unahusu ujifunzaji wa lugha ya pili na unapatikana katika taaluma ya Isimu Tumikizi. Tumejikita tu katika matatizo ya kimofolojia na kisintaksia. Sampuli zilitolewa kutoka wilaya ya Bomet. Jumla ya wanafunzi sitini walichunguzwa kutoka shule nne za msingi na Wanafunzi wa darasa la sita, saba na nane walihusika. Matokeo ya utafiti huu yanaonyesha kuwa makosa mengi ya kisarufi yanatokana na athari za lugha ya Kikipsigis. Makosa hayo pia yalihusu ujumlishaji mno wa baadhi ya maumbo ya sarufi ya Kiswahili.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/3583
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback