• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Usawiri wa Wahusika wa Kiume katika Riwaya za Kiswahili Zilizoandikwa na Wanawake

Thumbnail
View/Open
Fultext thesis (1.199Mb)
Date
2022
Author
Kanwa, Olivia
Metadata
Show full item record
Abstract
Utafiti huu ulishughulikia usawiri wa wahusika wa kiume katika riwaya za Kiswahili zilizoandikwa na wanawake. Utafiti umechunguza kazi za waandishi wa kike wa Kenya na wa Tanzania kwa kutumia mkabala linganishi. Malengo manne ya utafiti huu ni: kubainisha dhamira zinazowasilishwa na wahusika wa kiume, kuchanganua taswira zinazotumiwa na waandishi kuwasawiri wahusika wa kiume, kujadili mitazamo inayoibuliwa na wahusika wa kiume katika riwaya teule na kulinganisha na kulinganua waandishi wakike wa Kenya na Tanzania katika usawiri wao wa wahusika wa kiume. Riwaya mbili za waandishi wa kike wa Kenya ni Tumaini iliyoandikwa na Clara Momanyi, Dago wa Munje iliyoandikwa na Sheilla Ryanga na za kutoka Tanzania ni Kipimo cha Mizani ya Zainabu Burhani, Hiba ya Wivu ya Zainabu Mwanga zilihakikiwa kwa kufuata utaratibu. Sanjari na hilo, tasnifu hii imeonesha kuwa nadharia ya uhalisia, ujifunzaji wa kijamii (imejikita kwenye uana) na mwanaume mpya zimekuwa nadharia faafu zilizoongoza utafiti huu. Uhalisia umefafanuliwa kama msingi wa usawiri katika jamii kwa maana hutofautiana kulingana na hali na baina ya jamii moja na nyingine. Nadharia ya ujifunzaji wa kijamii huona tabia kama kitendo ambacho mtu hujifunza kutoka katika mazingira ambayo ndiyo hupelekea umuhimu wa majukumu ya kiuana. Mwisho, utafiti ulitumia nadharia ya mwanaume mpya, nadharia inayojaribu kuelezea kwanini baadhi ya wanaume hukaa na wake zao kwa usawa bila tabia za mfumo dume ambazo huashiria kuwepo kwa taasubi ya kuumeni. Nadharia hizi tatu zilitumika kujibu sehemu mbalimbali za maswali ya utafiti. Mbinu za utafiti zilizotumika ni usomaji wa riwaya teule kwa kina na kuhakiki. Kutokana na uhakiki, wahusika wa kiume wamesawiriwa chanya na waandishi wanawake. Wachache walikuwa hasi. Wameonesha pande mbili za wahusika kwa kuwachora hasi na chanya. Utafiti huu umesaidia kuongeza maarifa katika eneo la kijinsia na tahakiki za kifasihi.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/24256
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback