• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Mshabaha na Tofauti Kati ya Hadithi Fupi ya Kisasa na Ngano

Thumbnail
View/Open
Full text thesis (931.5Kb)
Date
2021
Author
Mwanzu, Misigo Daniel
Metadata
Show full item record
Abstract
Utafiti huu umeshughulikia mshabaha na tofauti kati ya hadithi fupi ya kisasa na ngano. Diwani zilizoshughulikiwa ni: Mwavyaji wa Roho na Hadithi Nyingine (Sanja, 2011), Kurudi Nyumbani na Hadithi Nyingine (Mbatiah, 2007) na Mimba Ingali Mimba na Hadithi Nyingine (Mc Onyango, 2006). Hali kadhalika, ngano zilizoshughulikiwa zimo katika vitabu vya Swahili Tales as Told by the Natives of Zanzibar (Steere, 1870) na Myths and Legends of the Swahili (Knappert, 1970). Utafiti ulilenga kuchanganua muundo, mtindo, maudhui na wahusika katika hadithi fupi ya kisasa na ngano. Nadharia iliyoongoza utafiti huu ni nadharia ya vikale iliyoasisiwa na Jung ama Frazer na kuimarishwa katika fasihi na Northrop Frye (1957) na baadaye ikaendelezwa na Campbell (2004), Guerin (2005) na Larsen (2018). Kulingana na Frye, kikale ni ishara ambayo huzua taswira inayojirudiarudia katika kazi ya sanaa kiasi kwamba inatambuliwa kama kiungo cha ujuzi wa mtunzi wa kazi fulani. Nadharia hii imeteuliwa kwa msingi kuwa ilituwezesha kuonyesha ikiwa taswira zinazojitokeza katika hadithi fupi zinasheheni picha kongwe zinazojirudiarudia mara kwa mara kama ilivyo katika ngano. Kwa msingi huu tumebaini kuwa kuna vigezo tofauti vya kupimia kazi za hadithi fupi na ngano. Aidha, utafiti huu umefanyika katika maktaba za vyuo vikuu nchini Kenya. Data ya kimsingi imepatikana kutokana na kusoma diwani ya hadithi fupi, ngano zilizomo katika vitabu vya Steere na Knappert, tasnifu, majarida na vitabu vinavyohusiana na mada ya utafiti. Data imechanganuliwa na kuwasilishwa kwa njia ya kimaelezo na lugha ya nathari kuambatana na malengo ya utafiti. Utafiti huu umeonyesha kuwa kuna tofauti nyingi kati ya hadithi fupi ya kisasa na ngano kuliko mshabaha. Hii inathibitisha kuwa hakuna hadithi fupi iliyotokana na ngano.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/22908
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback