• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Mnyambuliko wa vitenzi vya Lulogooli: mtazamo wa fonolojia leksia

Thumbnail
View/Open
Abstract (4.239Kb)
Date
2011-11-08
Author
Mayodi, David Adenya
Metadata
Show full item record
Abstract
Utafiti huu ulinuia kushughulikia mnyambuliko wa vitenzi vya Lulogooli. Lengo kuu lilikuwa kubainisha namna nadharia ya fonolojia leksia ifvyo toshelevu na mwafaka katika kushughulikia mnyambuliko huo. Utafiti ulifanywa kwenye taarafa ya Vihiga, Wilaya ya Vihiga katika Mkoa wa Magharibi, nchini Kenya. Jumla ya kata nne zilishirikishwa kwenye kazi hii nazo ni: Wamuluma, Mungoma, Maragoli ya kati na Maragoli kusini. Kata hizi zilishirikishwa kwa sababu inaaminika huko ndiko kuliko kitovu chao na kwamba lugha inayozungumzwa huko haijaathiriwa pakubwa na majirani zao. Utafiti ulikuwa na malengo manne ambayo ni kutambua na kubainisha taratibu za mnyambuliko wa vitenzi vya Lulogooli, kudhihirisha mifanyiko ya sauti inayoandamana na mnyambuliko huo, kubainisha kanuni na vigezo vinavyofuatwa kwenye mnyambuliko wake na kisha kutathmini maana mbalimbali zilizosetiriwa katika mnyambuliko huo. Utafiti umehusisha mbinu mbili kuu za utafiti yaani wa maktabani na nyanjani. Ili kufanikisha malengo yake, mazungumzo ya wasemaji wazawa wa lugha hii yalinaswa katika eneo la utafiti katika miktadha mbalimbali ili kupata vitenzi vinavyoeleza dhana na hali mbalimbali. Matokeo ya utafiti yamedhihirisha kwamba vitenzi vya Lulogooli vinanyambuliwa kwa namna maalum kwa kuzingatia sheria bayana za kifonolojia na unahusisha mabadiliko mbalimbali ya kifonolojia. Kazi hii imedhihirisha kuwa nadharia ya fonolojia leksia ni mwafaka katika kushughulikia mnyambuliko huo kwa kuzingatia mihimili yake ya nadharia hiyo.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/1615
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback