Repository logo
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Қазақ
  • বাংলা
  • हिंदी
  • Ελληνικά
  • Yкраї́нська
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
Repository logo
  • Communities & Collections
  • All of DSpace
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Қазақ
  • বাংলা
  • हिंदी
  • Ελληνικά
  • Yкраї́нська
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Wendo, Fadhili Hamisi"

Now showing 1 - 2 of 2
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Maudhui ya Ukungwi katika Nyimbo Teule za Taarab
    (East African Journal of Swahili Studies, 2025-07) Wendo, Fadhili Hamisi; Kaui, Titus
    Nyimbo za taarab zimetafitiwa na wataalam mbalimbali kwa mitazamo tofautitofauti. Kutokana na uchunguzi wa kina wa mtafiti, inabainika kuwa tafiti za awali kuhusu nyimbo za taarab, zimeegemezwa kwenye uchunguzi wa mafumbo katika taarab, masuala ya itikadi, nafasi ya mwanamke katika nyimbo za taarab usimulizi pamoja na uchanganuzi wa taswira katika nyimbo za taarab. Swala la jumbe za nyimbo za taarab kufungamana na mambo ya kijamii yakiwemo utamaduni limetajwa tu kijuujuu katika tafiti zao. Kutokana na upeku zi wa kina wa mtafiti, hakuna utafiti ambao umefanywa kuhusu dhima ya kungwi inavyotekelezwa na baadhi ya nyimbo za taarab. Utafiti huu ulihusu ubainishaji wa maudhui ya ukungwi katika nyimbo teule za taarab. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Simiotik i. Nadharia hii iliasisiwa na Ferdinand Dessaussure (1983) na Charles Pierce (1998) na inahusu uhusiano uliopo kati ya kitaja na kitajwa na matumizi ya ishara, picha na msimbo. Nguzo hii ilisaidia katika kufafanua mbinu za uwasilishaji wa ujumbe katika n yimbo teule za taarab. Data ya kimsingi iliyoichanganuliwa ilikuwa ya maktabani ambapo mtafiti alipakua nyimbo teule kutoka kwenye mtandao wa You Tube na kuzichanganua kwa kina. Matokeo yalionyesha kuwa kungwi ana jukumu la kuwafundisha wanawari kuhusu mas uala ya unyumba yakiwemo usafi wa mwili na nyumba, namna ya kumhudumia mume, namna ya kusema na marafiki na jamaa za mume, matumizi ya vifaa vya kiasili kama vile mbuzi, kinu, mchi ufagio miongoni mwa mengine. Aidha, maudhui haya ya ukungwi yanafundishwa n a waimbaji wa nyimbo teule za taarab
  • No Thumbnail Available
    Item
    Maudhui ya Ukungwi katika Nyimbo Teule za Taarab
    (Kenyatta University, 2025-11) Wendo, Fadhili Hamisi
    Utafiti huu umechunguza jinsi maudhui ya ukungwi yanavyojitokeza katika nyimbo teule za taarab. Malengo yafuatayo yalinuiwa kutekelezwa; kubainisha dhima ya kungwi katika jamii ya Waswahili, kuchunguza maudhui ya ukungwi katika nyimbo teule za taarab na kulinganisha dhima ya kungwi na maudhui ya ukungwi katika nyimbo teule za taarab. Sampuli iliteuliwa kimaksudi ambapo kati ya nyimbo nyingi za taarab, nne ndizo ziliteuliwa kutumika katika utafiti huu. Nyimbo hizi ni: Maji ya Uvuguvugu (Wachonga Vinyago), Nenda salama (Omar Kopa), Ndoa (Aslay na Khadija Kopa), Bi Harusi (AT). Sampuli ya utafiti huu iliteuliwa kwa kutumia mbinu ya kimakusudi. Kati ya maeneo mengi katika jamii ya Waswahili, eneo la Msambweni ndilo lililoteuliwa kutumika katika utafiti. Mbinu hii ilifaa katika kuwateua makungwi waliochangia data muhimu ya kuchanganuliwa. Utafiti huu uliongozwa na nadharia mbili; nadharia ya Simiotiki na nadharia ya Uamilifu. Nadharia ya Simiotiki iliasisiwa na Ferdinand Dessaussure (1913) na Charles Pierce (1977) na inahusu uhusiano uliopo kati ya kitaja na kitajwa na matumizi ya ishara, picha na msimbo. Nadharia hii ilisaidia katika kufafanua mbinu za uwasilishaji wa ujumbe katika nyimbo teule za taarab. Kwa upande mwingine nadharia ya Uamilifu iliasisiwa na Emile Dukheim (1912) na inahusika na uchambuzi wa dhima zinazojitokeza katika kazi za fasihi. Hii ilituongoza katika kubainisha dhima ya kungwi katika jamii. Utafiti huu ulikuwa wa kimaktaba na wa nyanjani ambapo maktabani; mtafiti aliweza kusoma tasnifu, makala na majarida yanayohusiana na mada. Nyanjani, mtafiti alitembelea eneo lengwa ili kuwahoji baadhi ya makungwi kuhusu dhima yao. Matokeo yalionyesha kuwa kungwi ana jukumu la kuwafundisha wanawali kuhusu maswala ya unyumba yakiwemo usafi wa mwili na nyumba, namna ya kumhudumia mume, namna ya kusema na marafiki na jamaa za mume, matumizi ya vifaa vya kiasili kama vile mbuzi, kinu, mchi ufagio miongoni mwa mengine. Aidha, maudhui haya ya ukungwi yanafundishwa na waimbaji wa nyimbo teule za taarab na kuonyesha namna kipera cha nyimbo na mawaidha vinaingiliana kimaudhui. Utafiti huu unatarajiwa kutoa mchango wa kuonyesha jinsi vitanzu vya mawaidha na nyimbo huingiliana kidhima.

DSpace software copyright © 2002-2026 LYRASIS

  • Cookie settings
  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback