Uhusiano wa mikakati ya ufundishaji wa fasihi ya watoto ya kiswahili na umilisi wa kusoma katika shule za msingi, kasarani, kaunti ya Nairobi, Kenya

Loading...
Thumbnail Image
Date
2016-10
Authors
Chacha, Selina Rhobi
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Kenyatta University
Abstract
IKISIRI Fasihi ya watoto ina manufaa katika ukuzaji wa umilisi wa lugha shuleni na hata katika mazingira ambayo si ya shule. Licha ya manufaa hayo, baadhi ya wanafunzi hawasomi vitabu vya hadithi. Kutopenda kusoma kunaweza kuwa kumesababishwa na mikakati inayotumiwa na walimu katika ufundishaji wa vitabu hivyo vya fasihi. Lengo la utafiti huu ni kuchanganua mikakati inayotumiwa katika ufundishaji wa fasihi na umilisi wa kusoma miongoni mwa wanafunzi wa shule za msingi za ya Kasarani. Utafiti huu ulichanganua vifaa vya kufundishia na kutathmini kazi ya wanafunzi. Aidha, utafiti uliongozwa na nadharia ya semiotiki ambayo hujengwa kwa miundo ishara. Mwanzilishi wa nadharia semiotiki alikuwa Charles Piece. Muundo wa utafiti huu ulikuwa wa usoroveya elezi. Mbinu bahatishi ilitumiwa kuteua shule za msingi za umma wilayani Kasarani. Mbinu kusudi ilitumiwa kuteua walimu wa Kiswahili kumi na wawili wanaofundisha darasa la saba. Mbinu bahatishi ilitumiwa kuteuwa wanafunzi sitini katika kila darasa. Insha sitini za wanafunzi katika shule ziliteuliwa na kuchanganuliwa ili kutathmini umilisi wa kusoma miongoni mwa wanafunzi. Vifaa vilivyotumiwa katika utafiti ni hojaji na mahojiano kwa walimu, kutazama somo darasani na kutathmini insha za wanafunzi. Data ilichanganuliwa kwa kutumia tarakilishi, ili kupata uwiano na wastani. Matokeo ya utafiti yaliwasilishwa kwa kutumia maelezo, majedwali na michoro. Kutokana na utafitii, asili mia moja ya walimu waliripoti kuwa kusoma kwa kimya na wa kipekee ni mikakati mikuu wanayoitumia kufunza fasihi. Utafiti pia ulibaini kuwa, asili mia moja ya walimu walitumia vitabu vya hadithi na ubao katika ufundishaji. Vifaa vya teknolojia ya kisasa havikutumiwa. Matokeo ya utafiti huu yalionyesha kuwa wanafunzi hawakufanya vizuri katika insha zao kwasababu walimu hawakutumia mikakati tofauti tofauti na vifaa vya teknolojia ya kisasa. Walimu wanatakikana kutumia mikakati tofauti tofauti na vifaa vya teknolojia ya kisasa katika ufundishaji ili kuimarisha matokeo ya lugha ya Kiswahili. Utafiti huu ulikuwa wa manufaa kwa walimu, wanafunzi, wakuzaji mitaala na watafiti wa fasihi ya watoto. ABSTRACT Children literature is an important aspect in children’s language performance in school and life after school. Despite its critical role, pupils are not reading enough literature books for them to master language. The purpose of this study was to analyse the teaching strategies used to teach children literature and reading competence among class seven pupils at Kasarani Sub-County, Nairobi County. The study aimed at achieving the following objectives: to analyse the teaching strategies used by teachers to teach children literature; to analyse resources used in teaching children literature; and to evaluate children’s reading comptence in literature. This research was guided by Semeotic Theory. The design of the study was descriptive survey. Simple random sampling was used to sample twelve schools in Kasarani and purposive sampling was used to select twelve Kiswahili teacher’s handling children literature in class seven. Questionnaires, interview guides, observation and document analysis were used to collect data. The collected data was edited, organized, entered into a computer and analyzed with the aid of Social Package for Social Sciences (SPSS). The analysed data was presented using descriptive statististics such as tables, graphs and charts. The findings of this study indicated that silent and individual reading were the major strategies used in teaching liteature in most primary schools, thus, teachers did not use variety of teaching strategies. All teachers (100%) agreed that story books and writing boardswere the major resources used in delivering children literature. The study concludes that new instructional techniques such as redio lessons, televisions, recorded videos and audios were not utilized at all. Majority of pupils, as well, did not perform well in all sections of composition.This is because the teachers did not use different strategies and new instructional techniques in their teaching to improve pupils performance. The study recommends that; teachers should use different strategies in teaching children’s literature, children should be encouraged to read more story books, and library lessons should be more than one
Description
Tasnifu hii imewasilishwa kutosheleza baadhi ya mahitaji ya shahada ya uzamili katika idara ya mawasiliano na teknolojia ya elimu, shule ya elimu, Chuo Kikuu cha Kenyatta. October, 2016 Call No. PL 8703.5 .K4C48
Keywords
Swahili literature
Citation