Repository logo
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Қазақ
  • বাংলা
  • हिंदी
  • Ελληνικά
  • Yкраї́нська
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
Repository logo
  • Communities & Collections
  • All of DSpace
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Қазақ
  • বাংলা
  • हिंदी
  • Ελληνικά
  • Yкраї́нська
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Jepkemboi ,Anne"

Now showing 1 - 1 of 1
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Mielekeo ya Wauza Mifugo Mnadani Wanaozungumza Kinandi Kuhusu Kiswahilikatika Kaunti ya Nandi
    (Kenyatta University, 2025-11) Jepkemboi ,Anne; King'ei, Kitula Osore, Miriam
    Utafiti huu ulilenga kueleza jinsi mielekeo ya wauza mifugo mnadani katika kaunti ya Nandi kuhusu lugha ya Kiswahili inavyoathiri matumizi yao ya lugha. Mwelekeo wa watu kuhusu vitu au dhana unaweza kuathiri wale watu au dhana hizo. Tafiti tofauti zilizofanywa kuhusu mielekeo ya watu kwa lugha zimebaini kuwa mielekeo ya watu huweza kuwa hasi au chanya kutegemea masiala mbalimbali kama vile elimu, umri, mazingira, jinsia na kadhalika. Utafiti huu uliongozwa na malengo yafuatayo: kupambanua mielekeo ya wauza mifugo mnadani wanaozungumza Kinandi kwa lugha ya Kiswahili katika kaunti ya Nandi; kubainisha mambo ambayo husababisha mielekeo ya wauza mifugo mnadani wanaozungumza Kinandi kuhusu lugha ya Kiswahili na kuchunguza athari ya mielekeo hiyo ya lugha kwa maendeleo ya Kiswahili katika jamii hii. Nadharia ya Utendaji Razini (Theory of Reasoned Action) iliyoasisiwa na Fishbein na Ajzen (1975) ilitumiwa kuongoza utafiti huu. Wataalamu hawa wanasema kuwa binadamu ni viumbe wanaofikiria na wanajua aina ya mielekeo na tabia walizo nazo. Kwa hivyo, maelezo ya watafiti hawa yanalingana na lengo la utafiti huu ambalo ni kueleza matumizi ya Kiswahili miongoni mwa wauza mifugo mnadani ambao mielekeo yao hudhihirika kupitia matumizi yao ya lugha. Utafiti huu ulihusisha wauza mifugo 35 kutoka minada yote 7 katika kaunti ya Nandi. Mtafiti alitumia idadi hii kimaksudi. Utafiti huu ulitumia mbinu ya utafiti wa maelezo ambapo data ilikusanywa kupitia hojaji, mahojiano na kushiriki utendaji kisha ikachanganuliwa na kuwasilishwa kupitia majedwali, baa grafu na pai chati. Ilibainika kwamba wauza mifugo mnadani wana mitazamo hasi kuhusu utumiaji wa Kiswahili kwa sababu wanahisi Kiswahili ni kigumu kwao. Matokeo ya utafiti huu yanaweza kutumiwa na washikadau mbalimbali wanaohusika na lugha ili kuweka mikakati ya kuhakikisha kuwa Wakenya wote wanafahamu na kutumia kwa ufasaha lugha ya Kiswahili ili wabadili mielekeo yao hasi kuhusu lugha hii.

DSpace software copyright © 2002-2026 LYRASIS

  • Cookie settings
  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback