Kutathmini Mafunzo Tafsiri katika Matini za Kidini: Mfano wa Njia Salama

Loading...
Thumbnail Image
Date
2023
Authors
Nyabunga, Vince Arasa
Osore, Miriam
Mwita, Leonard Chacha
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
EANSO
Abstract
Tafsiri imekuwa njia ya kuhamisha maarifa na ujumbe kutoka lugha moja hadi nyingine kwa muda mrefu lakini imetambuliwa kama taaluma ya kiusomi siyo miaka mingi iliyopita (Munday, 2001). Tafsiri zilizopo zimefanywa kwa kuzingatia mtazamo wa ulinganifu wa visawe vya lugha chanzi na lugha pokezi bila kuhusisha dhana ya uelewaji na ufasiri wa hadhira lengwa. Utafiti huu ulivuka mtazamo huo na kuchunguza uelewaji na ufasiri wa mafunzo tafsiri katika Njia Salama. Matini za kidini hutumiwa katika maeneo ya maabadi ili kuadilisha, kukuza mahusiano na kutangamanisha jamii. Vilevile, huwasilisha mafunzo muhimu ya kihistoria ya kidini ambayo yanafaa kueleweka na kufasirika kwa njia ya wazi. Hata hivyo, uchanganuzi wa awali wa matini tafsiri, unaonyesha kuwepo kwa matatizo ya uelewaji na ufasiri wa ujumbe wa hali ya maisha na uinjilisti. Kwa hivyo, lengo la utafiti huu ni kuthamini mafunzo hayo na kubainisha namna matatizo hayo yanavyojitokeza. Hali kadhalika, utafiti huu unakusudia kuthibitisha iwapo matatizo ya uelewaji na ufasiri wa ujumbe katika matini teule yanasababishwa na tofauti za kiisimu, kimtindo, kimuundo na kitamaduni baina ya lugha asilia na lugha pokezi. Katika kutekeleza jukumu hili, washiriki 140 walishirikishwa kutoa data ya utafiti. Data iliyopatikana ilichanganuliwa kwa njia ya kimaelezo na kitakwimu. Kwa hivyo, viongozi 42 na waumini 98 kutoka kanisa saba teule walishiriki. Washiriki waliojua kusoma na kuandika lugha ya Kiswahili walisailiwa na kuhojiwa. Nadharia ya skopos inayoweka mkazo kwenye matini tafsiri iliongoza utafiti huu. Matokeo ya utafiti huu yalilenga kuchangia uelewaji na ufasiri wa ujumbe katika matini tafsiri za kidini
Description
Article
Keywords
Hali ya Maisha, Uinjilisti, Skopos
Citation
Nyabunga, V. A., Osore, M & Mwita, L. C. (2023). Kutathmini Mafunzo Tafsiri katika Matini za Kidini: Mfano wa Njia Salama. East African Journal of Swahili Studies, 6(1), 1-15. https://doi.org/10.37284/jammk.6.1.1036.