Usawiri wa mishororo katika ushairi wa Kiswahili

Loading...
Thumbnail Image
Date
2016
Authors
Ndirangu, Teresa Wanjiku
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Kenyatta University
Abstract
Utafiti huu ulitathmini kuchunguza usawiri wa mishororo katika ushairi wa Kiswahili. Diwani mbili zilirejelewa: Tamthilia ya Maisha (2005) iliyohaririwa na Kyallo Wadi Wamitila na Diwani ya Karne Mpya (2007) ambayo imehaririwa na Ken Walibora. Utafiti huu ulidhamiria kutimiza malengo matatu makuu. Kwanza, tulilenga kuainisha mishororo katika mashairi teule kutoka diwani hizo. Pili, kuchunguza dhima mbalimbali za mishororo hiyo. Aidha, tulilenga kuchunguza jinsi usawiri wa mishororo ulivyofanikisha usawiri wa dhamira na maudhui. Nadharia ya Kiutanzu iliongoza utafiti huu ambapo mihimili yake ilitumiwa kuhakiki mishororo kama sifa ya msingi ya utanzu wa ushairi. Imetusaidia kuhakiki sura mbalimbali za mishororo na nafasi zake katika usawin wa mashairi. Data ilikusanywa kwa kusoma kwa kina na kunukuu mistari iliyotuelekeza kwenye malengo ya utafiti wetu. Data hiyo imechanganuliwa na kuwasilishwa kwa mbinu ya kimaelezo kuambatana na malengo, maswali ya utafiti na nadharia iliyozingatiwa. Uwasilishaji umefanywa kwa sura tano. Sura ya kwanza ina sehemu zifuatazo: utangulizi, mada ya utafiti, sababu za kuchagua mada, upeo na mipaka, yaliyoandikwa kuhusu mada na misingi ya nadharia. Sura ya pili imechunguza historia na mabadiliko ya ushairi wa Kiswahili. Sura ya tatu imelenga kuainisha mishororo na sura ya nne imeshughulikia dhima za mishororo hiyo. Sura ya tano imeshughulikia muhtasari, hitimisho na mapendekezo ya utafiti. Matokeo ya utafiti huu yatawafaa wanafunzi, wahakiki na watunzi wa mashairi kwa jumla.
Description
Tasnifu hii imetolewa ill kutosheleza baadhi ya mahitaji ya shahada ya uzamili katika chuo Kikuu cha Kenyatta
Keywords
Citation