• Login
    View Item 
    •   Repository Home
    • Master Theses and Dissertations(MST)
    • MST-School of Education
    • MST-Department of Educational Psychology
    • MST-Department of Educational Psychology
    • View Item
    •   Repository Home
    • Master Theses and Dissertations(MST)
    • MST-School of Education
    • MST-Department of Educational Psychology
    • MST-Department of Educational Psychology
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Matumizi ya masimulizi na malumbano katika tamthilia ya kiswahili

    Thumbnail
    View/Open
    Mwambi Phoebe.pdf (6.898Kb)
    Date
    2011-08-12
    Author
    Wakesho, Mwambi Phoebe
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Utafiti huu umeshughulikia matumizi na malumbano katika tamthilia ya Kiswahili. Tamthilia zilizoshughulikiwa ni Wingu jeusi(1987) na pango(2003). Utafiti huu uliongozwa na nadharia mseto za uhakiki wa mwingilianomatini. Nadharia hizi zilifaa katika utafiti huu, hasa ikizingatiwa kwamba tmthilia hizi zilizotafitiwa zimesheheni matumizi ya masimulizi na malumbano. Tasnifu hii ina sura tano. Sura ya kwanza ni utangulizi wa utafiti. Hapa mtafiti ameshughulikia mada ya utafiti,sababu ya kuchagua mada na yaliyoandikwa kuhusu mada hii. Pia amejadili upeo na mipaka ya utafiti huu na misingi ya nadharia zilizoongoza utafiti huu. Mwisho, mbinu za utafiti zimeelezwa. Sura ya pili imejadili asili ya fasihi, fasihi andishi sifa za tamthilia na mikondo yake, tofauti simulizi na andishi na maathiriano ya fasihi andishi na simulizi. imebainika kwamba waandishi wengine huathiriwa kifani, kimaudhi na kidhamira. Katika sura hii imebainika kwamba fasihi andishi haijavumbua dhamira mpya. Pia imebainika kwamba michezo mingi ya redio ambayo hupendwa sana na wasikilizaji ni fasihi simulizi. Utafika ulidhamiria kuhakiki jinsi fasihi simulizi inavyoiathiri tamthilia ya kiswahili katika kutumia masimulizi na malumbano kama mtindo wa uandishi. Sura ya tatu imechunguza jinsi wa masimulizi ulivyotumiwa katika tamthilia ya kiswahili. Pia sura hii imejadili historia fupi za waandishi wa tamthilia za wingu jeusi na pango ambao ni chacha na wamitila. Vile vile mihtasiri ya tamthilia za wingu jeusi na pango imeonyeshwa ili kumpa mtafiti mwelekeo kuhusu falsafa ya waandishi hawa. Sura ya nne imechunguza matumizi ya mtindo wa malumbano katika tamthilia za wingu jeusi na pango. Utafiti umebainisha kwamba malumbano huweza kusababishwa na maswala ya kijamii, kisiasa,kiuchumi,kidini na kadhalika. Pia imebainika kwamba malumbano huweza kuwa na athari hasi kama vile kukasirika,kutukanana,kudharauliana na kadhalika. Sura ya tano imejadili muhtasari wa utafiti huu. Pia imeonyesha matokeo ya utafiti, matatizo ya utafiti, mchango wa utafiti huu na mapendekezo ya mtafiti. Mwishowe kuna marejeleo ya utafiti huu. Utafiti huu pia ni miongoni mwa kazi chache ambazo zimewahi kuhakiki tamthilia za wingu jeusi na pango kwa kuzihusisha na vipera vya fasihi simulizi na pia kuzihakiki kwa kuzingatia nadhria mseto za uhakiki wa kimtindo na mwingilianomatini. Utafiti huu utawasaidia wahadhiri na wanafunzi wa vyuo vikuu,n pia wanafunzi wa shule za upili,kwani somo la kiswahili linahusisha fasihi simulizi na andishi. Pia mtafiti anaamini kwamba utafiti huu utawafaidia wapenzi wote wa lugha ya kiswahili.
    URI
    http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/755
    Collections
    • MST-Department of Educational Psychology [190]

    Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
    Contact Us | Send Feedback

     

     

    Browse

    All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
    Contact Us | Send Feedback