• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Lugha ya wanawake wakikuyu inavyoimarishwa ubabedume katika maongezi ya kawaida

Thumbnail
View/Open
Abstract (45.65Kb)
Date
2012-03-29
Author
Muchiri, Patrick Maina
Metadata
Show full item record
Abstract
Utafiti huu ulilenga kubainishajinsi wanawake Wakikuyu wanavyouimarisha ubabedume kupitia maongezi yao ya kawaida. Nadharia ya Tahakiki Usemi imekuwa nanga ya uchanganuzi wa matumizi ya lugha kutokana na msisitizo wake wa muktadha katika kueleweka kwa matamshi. Sarufi Amilishi Mfumo imejaliza uchanganuzi kupitia msisitizo wake wa mfumo wa maana za matamshi. Utafiti ulifanywa maktabani na pia nyanjani. Maktabani, data ya upili ilitumiwa ili kufanikisha utafiti wa nyanjani. Nyanjani, maongezi halisi ya wanawake kuhusu wanaume yalizingatiwa hasa sokoni, na kwenye vikundi vya wanawake. Uwasilishaji wa data utakuwa wa kimaelezo kupitia sura tano. Sura ya kwanza imejenga utangulizi ikihusisha vipengele vya kimsingi vya utafiti. Utamadunijamii wa Wakikuyu umeshughulikiwa katika sura ya pili pamoja na vipengele vyake vinavyokuza ubabedume. Taswira ya mwanamume na taswira ya mwanamke zimefafanuliwa na mifano halisi ya kimaongezi kutolewa katika sura ya tatu na ya nne mtawalia. Ufafanuzi wa maana za taswira hizi ulikitwa katika miktadha ya matumizi ya lugha kama inavyoelekeza nadharia inayotumiwa katika utafiti huu. Sura ya tano imehitimisha utafiti kwa kutoa matokeo ya utafiti, mahitimisho ya utafiti pamoja na mapendekezo ya utafiti zaidi. Utafiti huu unatarajiwa kuwanufaisha wanaisimu, wasomi wa masuala ya kijinsia, na wanawake kwa jumla. Pia unatarajiwa kusaidia katika uzinduzi wa jamii kuhusu matumizi ya lugha na athari zake kimawasiliano.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/3584
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [233]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback