• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Tathmini ya Ufundishaji na Ujifunzaji wa Somo la Imla katika Shule za Upili: Gatuzi la Trans-Nzoia, Kenya

Thumbnail
View/Open
Fultext thesis (1.291Mb)
Date
2021
Author
Lonah, Kurema Aoko
Metadata
Show full item record
Abstract
Utafiti huu ulitathmini ufundishaji na ujifunzaji wa somo la imla katika shule za upili katika Gatuzi la Trans-Nzoia. Utafiti huu ulilenga kubainisha vipengele vya stadi ya uandishi ambavyo wanafunzi hujifunza katika somo la imla, mbinu ambazo walimu hutumia kufundishia somo la imla, changamoto zilizowakumba walimu katika ufunzaji wa imla na udhaifu uliojitokeza katika ufundishaji na ujifunzaji wa somo hilo na kupendekeza namna ya kuliboresha. Uteuzi wa sampuli kusudi ulitumiwa kuchagua gatuzi lililohusishwa katika utafiti huu. Shule zilizotafitiwa ziliteuliwa kwa kutumia sampuli tabakishi na bahatishi. Nadharia zilizoongoza utafiti huu ni Nadharia ya Lugha Mawasiliano iliyoasisiwa katika miaka ya 1960 na Nadharia ya Uchanganuzi Makosa ya Corder (1967). Mihimili ya Nadharia ya Lugha ya Mawasiliano ilitumiwa kuchanganua mbinu za ufundishaji wa somo la imla ilhali Nadharia ya Uchanganuzi Makosa ilitumiwa kudhihirisha vipengele vya stadi ya kuandika katika somo la imla na udhaifu katika ujifunzaji wa somo hilo katika shule za sekondari. Utafiti huu ulifanywa nyanjani. Mbinu za mahojiano na uchunzaji zilitumiwa kukusanya data. Data hiyo imewasilishwa kutumia maandishi ya nathari, majedwali na vielelezo. Matokeo yamebaini kuwa walimu wengi katika shule za sekondari wanafundisha somo la imla kijuujuu bila kufanya maandalizi ya kimaksudi. Aidha, utafiti huu umeonyesha kuwa wanafunzi wanajifunza vipengele mbalimbali vya lugha kama vile hijai, sarufi, hati bora, msamiati na matamshi bora katika somo la imla. Utafiti huu unapendekeza walimu waandaliwe warsha mbalimbali za Kiswahili ili wahamasishwe kuhusu mbinu mbalimbali za kufundishia somo la imla. Aidha, silabasi ya Kiswahili ifanyiwe marekebisho ili kuwezesha maandalizi ya kimaksudi ya ufundishaji wa imla. Isitoshe, utafiti huu unapendekeza tume ya kuwaajiri walimu (T.S.C) iwaajiri walimu zaidi na kuwaruhusu walimu wa Kiswahili kufundisha Kiswahili lugha na Fasihi pekee ili kuwapa walimu muda wa kutosha wa kufundisha vipengele vyote vya stadi za lugha.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/23374
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback