• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Mchango wa fasihi simulizi katika fasihi andishi: mfano wa visasili katika Mafuta (1984) na Walenisi (1995)

Thumbnail
View/Open
Full text thesis (511.3Kb)
Date
2017-09
Author
Okemwa, Milkah Kerubo
Metadata
Show full item record
Abstract
Utafiti huu ulitathmini mchango wa fasihi simulizi katika fasihi andishi. Utafiti ulilenga kubainisha umuhimu wa visasili katika utunzi wa riwaya ya Kiswahili. Malengo ya utafiti yalikuwa ni kuonyesha ubainikaji wa visasili, mchango na umuhimu wake katika utunzi wa riwaya ya Mafuta (1984) na Walenisi (1995). Riwaya hizi ziliandikwa na Katama Mkangi. Utafiti uliongozwa na nadharia ya mwingilianomatini iliyoasisiwa na mwananadharia Kristeva (1966). Kuingiliana kwa matini katika kazi ya fasihi kuna maana ya kazi moja ya kifasihi kuwa na sifa za tanzu nyingine ndani yake ili kupitisha ujumbe. Visasili viliteuliwa kimakusudi kwa mujibu wa malengo ya utafiti. Utafiti ulifanywa maktabani kwa kusoma vitabu viteule kwa kina, miswada, majarida, tasnifu na makala mbalimbali yenye data iliyohusu mada hii. Mtafiti pia alizingatia matumizi ya mtandao ili kupata ujumbe zaidi. Ukusanyaji wa data ulifanywa kwa kuongozwa na nadharia ya utafiti. Aidha, data ilichanganuliwa kwa kuainishwa kwa misingi ya ubainishaji wa visasili, mchango na umuhimu wake. Kisha, uchanganuzi wa data uliongozwa na maswali ya utafiti, malengo ya utafiti na mihimili ya nadharia. Matokeo ya utafiti yaliwasilishwa kwa mbinu ya kimaelezo na kwa kutoa mifano mwafaka ya aina za visasili katika riwaya teule.Tunatumai kwamba kazi hii itatoa mchango maalum kwa wanafunzi, walimu, wahakiki wa fasihi, wasomi pamoja na wakuza mitaala kwa kuwapa mwanga zaidi kuhusu mchango wa fasihi simulizi katika kukuza na kuendeleza uhakiki wa riwaya teule. Kadhalika, unaangazia suala la kuchanganua visasili kama kipengele cha mwingilianomatini katika ufundishaji na ujifunzaji wa riwaya.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/18618
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback