• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Grafolojia katika uchapaji wa riwaya ya mkamandume

Thumbnail
View/Open
Full text thesis (567.8Kb)
Date
2017
Author
Musotsi, Eliud Teyie
Metadata
Show full item record
Abstract
Utafiti huu ulichunguza mchango wa vipengele vya kigrafolojia katika uchapaji wa riwaya ya Mkamandume ya Said A. Mohamed. Uliviangazia vipengele hivyo kwa kutathmini jinsi vilivyotumika na athari kwa msomaji wa riwaya teule na utanzu wa riwaya kwa jumla. Utafiti uliongozwa na nadharia ya kimtindo iliyoasisiwa na Baally (1909) na kuenezwa na Jakobson (1958) na Halliday (1971) na kisha kuelezewa na akina Leech na Short (1981). Aidha, mitazamo ya Leech na Short (1981) ilizingatiwa zaidi. Kulingana nao, mojawapo ya dhana ya kimtindo inahusu matumizi ya vipengele vya kigrafolojia kama vile viakifishi, herufi kubwa, tahajia, mlazo na hata kugawika kwa maandishi kwa aya kadha miongoni mwa vipengele vingine vya kiisimu. Kiupeo, utafiti huu ulijikita katika riwaya ya Mkamandume, na ulishughulikia vipengele hivyo vya kigrafolojia riwayani. Utafiti ulifanyiwa maktabani ambamo nilisoma kwa kina vitabu mbalimbali kuhusu mada na nadharia ya kimtindo. Data iliyokusanywa, ilichanganuliwa kulingana na malengo ya utafiti pamoja na msingi wa nadharia ya kimtindo. Data hiyo iliwasilishwa kwa njia ya kimaelezo. Ripoti ya utafiti ilipangwa katika sura tano. Sura ya kwanza ilijumulisha utangulizi ambamo usuli wa mada ya utafiti, suala, maswali ya utafiti, malengo, sababu za kuchagua mada, upeo na mipaka, yaliyoandikwa kuhusu mada, msingi wa nadharia, pamoja na mbinu za utafiti zilirejelewa. Sura ya pili iliangazia riwaya ya kisasa katika miktadha ya Kimagharibi na Uswahilini. Sura ya tatu iliihakiki riwaya ya Mkamandume huku vipengele vya kigrafolojia; viakifishi vilivyotumika na mwandishi vikijadiliwa. Katika sura ya nne tulijadili vipengele vingine vya kigrafolojia visivyokuwa viakifishi ambavyo mwandishi alivitumia katika ujenzi wa riwaya huku athari yavyo ikichanganuliwa. Sura ya tano ilijumulisha ufupisho wa yaliyotangulia. Utafiti huu ulilenga kuwanufaisha wanafunzi, wasomaji, wahakiki na wandishi wa riwaya kwa ujumla.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/18587
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback