• English
    • français
  • English 
    • English
    • français
  • Login
View Item 
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
  •   Repository Home
  • Master Theses and Dissertations(MST)
  • MST-School of Humanities and Social Sciences
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages
  • View Item
JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

Viwango vya uhalisi na ubunifu ka tika riwaya teule za Kiswahili

Thumbnail
View/Open
fulltext (76.05Mb)
Date
2014-09-11
Author
Lomatoro, Joel P.
Metadata
Show full item record
Abstract
Katika utafiti huu, tumeshughulikia viwango vya uhalisi na ubunifu katika riwaya teule za Kiswahili: Cheche za Moto (2008) ya Habwe John, Kaburi BUa Msalaba (1969) ya Kareithi P.M. na Kusadikika (1951) ya Shaaban Robert.IIi kuafiki hili, tumeangalia mbinu zilizotumiwa na waandishi kusawiri uhalisia na ubunifu katika riwaya za Kiswahili. Kila mwandishi ana njia yake ya kipekee ya kuwasilisha kazi yake. Kuna wanaoeleza yaliyotendeka katika jamii kwa uaminifu na kwa narnna ambayo atakayesoma kazi yake ataona ni mambo yanayosadikika au yaweza kutendeka katika jamii. Njia zinazotumiwa na waandishi kama hao zimeangaziwa katika utafiti huu. Zaidi ya hayo kuna waandishi wanaovuta fikra zao na kusimulia visa ambavyo vinaonekana kuwa ni vya kufikirika tu wala haviwezi kutendeka katika ulimwengu halisi. Kazi hizo ndizo tumeita 'ubunifu' katika utafiti huu. Hivyo basi kazi hii imejaribu kuangazia mbinu hizo na kuona iwapo kuna uhusiano wowote kati ya kazi hizo za kihalisia na kibunifu. Katika kuangalia uhusiano huo, utafiti huu umeangalia namna ambavyo waandishi wa rriwaya zilizotajwa, wameeleza visa 'kibunifu' na namna ambavyo uhalisia unajitokeza katika 'ubunifu' huo. 'Ubunifu' unaojitokeza katika kazi za kihalisi pia umeangaziwa. Nadharia iliyotumiwa ni nadharia ya uhalisia. Nadharia hii imechaguliwa kwa misingi kuwa mihimili yake itatuwezesha kuchambua vitabu vilivyoteuliwa na kuafiki malengo ya utafiti. Data ya utafiti ilipatikana kwa kusoma vitabu vyote vilivyochaguliwa na yaliyoangaliwa ni namna waandishi wamewasawiri wahusika wao, matukio na mandhari yao. Uchanganuzi ulifanywa kwa njia ya maelezo na mahitimisho kutolewa kimaelezo. Utafiti huu umeeleza nafasi ya uhalisi na ubunifu katika maendeleo ya riwaya za Kiswahili. Utatoa mchango katika uchambuzi wa riwaya za Kiswahili na matokeo yake kutumiwa katika kuainisha riwaya hizo.
URI
http://ir-library.ku.ac.ke/handle/123456789/11227
Collections
  • MST-Department of Kiswahili and African Languages [234]

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback

 

 

Browse

All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

My Account

LoginRegister

Designed by Library ICT Team copyright © 2017 
Contact Us | Send Feedback